Wednesday 31 May 2017

Walimu Wilaya ya Siha watakiwa kutimiza wajibu wao




Walimu Wilayani Siha Watakiwa kutimiza wajibu wao
Walimu wa shule za msingi na Sekondari Wilaya ya Siha Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kutimiza wajibu wao wa kazi ili kuongeza ufaulu wa Wanafunzi katika shule wanazofundisha.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu katika maazimisho ya juma la elimu yaliyofanyika Kiwilaya  katika shule ya msingi Sanya Juu tarehe 30.5.2017.

Mkuu wa Wilaya ya Siha ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika maazimisho ya elimu kwa mwaka 2017 Wilayani Siha, alikagua maonesho mbalimbali ya wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari na kuridhishwa na kazi zilizoonyeshwa na wanafunzi.

Katika hotuba aliyoitoa kwa Wananchi,wadau wa elimu,Walimu na Wanafunzi ,Mkuu  wa Wilaya ya Siha aliwataka Walimu kutimiza wajibu wao na kutambua kuwa wao kama watumishi wa Umma ni sehemu muhimu ya Serikali.

Aliongeza kuwa Serikali ya awamo ya Tano chini ya uongozi thabiti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli inawathamini sana walimu na inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Walimu katika kulikomboa Taifa na adui ujinga.

Aidha,Mhe Onesmo Buswelu aliwataka wazazi kuendelea kushirikiana na Serikali yao kwa lengo la kuhakikisha kuwa watoto wa Kitanzania wanapata elimu inayostahili kwa maendeleo ya familia,jamii na taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment