OFISI
YA RAIS TAMISEMI
HALMASHAURI YA
WILAYA YA SIHA
TAARIFA KWA UMMA
Ofisi
ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro
inapenda kuujulisha Umma kuwa taarifa iliyotolewa na gazeti la Nipashe la tarehe 23 Mei,2017 yenye kichwa cha
maneno “Viwanja Vyageuzwa Mashamba Kodi”
Ofisi
ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Siha inapenda kuufahamisha Umma kuwa
taarifa iliyotolewa siyo sahihi na ilikuwa na lengo la kuupotosha Umma na
kuwapa hofu wanaomiliki viwanja Siha. Ukweli wa jambo hili ni kuwa eneo lililokodishwa
na Halmashauri lenye ukubwa wa hekari
767 siyo eneo la viwanja kama
ilivyoandikwa na gazeti tajwa hapo juu, bali eneo hili lilitengwa na
Halmashauri ya Siha kwa ajili ya shughuli za uwekezaji.
Aidha,Ofisi
ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Siha inapenda kufahamisha Wananchi wote
wanaomiliki viwanja vilivyopimwa katika
Halmashauri ya Siha kuwa viwanja vyao vipo salama na Halmashauri haijawahi
kubadilisha matumizi ya ardhi hiyo.
Hata
hivyo,Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Siha inatoa wito kwa
Wananchi wote wanaomiliki viwanja katika eneo la Halmashauri kuviendeleza
viwanja wanavyomiliki.
Imetolewa na:-
Zakayo
Elifaison
Mkuu wa
Kitengo cha Habari & Mawasiliano Halmashauri (W) Siha
24 Mei,
2017
No comments:
Post a Comment