Walimu Wilayani
Siha Watakiwa kutimiza wajibu wao
Walimu wa shule za msingi na Sekondari Wilaya
ya Siha Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kutimiza wajibu wao wa kazi ili kuongeza
ufaulu wa Wanafunzi katika shule wanazofundisha.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Siha
Mhe.Onesmo Buswelu katika maazimisho ya juma la elimu yaliyofanyika Kiwilaya katika shule ya msingi Sanya Juu tarehe 30.5.2017.
Mkuu wa Wilaya ya Siha ambaye pia alikuwa
mgeni rasmi katika maazimisho ya elimu kwa mwaka 2017 Wilayani Siha, alikagua
maonesho mbalimbali ya wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari na kuridhishwa
na kazi zilizoonyeshwa na wanafunzi.
Katika hotuba aliyoitoa kwa Wananchi,wadau wa
elimu,Walimu na Wanafunzi ,Mkuu wa Wilaya
ya Siha aliwataka Walimu kutimiza wajibu wao na kutambua kuwa wao kama
watumishi wa Umma ni sehemu muhimu ya Serikali.
Aliongeza kuwa Serikali ya awamo ya Tano
chini ya uongozi thabiti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli inawathamini
sana walimu na inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Walimu katika kulikomboa
Taifa na adui ujinga.
Aidha,Mhe Onesmo Buswelu aliwataka wazazi
kuendelea kushirikiana na Serikali yao kwa lengo la kuhakikisha kuwa watoto wa
Kitanzania wanapata elimu inayostahili kwa maendeleo ya familia,jamii na taifa
kwa ujumla.