Siha yang’ara
michezo ya UMISSETA Mkoa wa Kilimanjaro
Timu ya Michezo ya wanafunzi wa shule za
sekondari Wilaya ya Siha imekuwa tishio kwa michezo mbalimbali kwa mkoa wa
Kilimanjaro iliyomalizika hivi karibuni mjini Moshi.
Katika michezo hiyo Timu ya Wilaya ya Siha imefanikiwa kutangazwa mabingwa
wa Mkoa wa Kilimanjaro katika michezo ifuatayo:-
i)
Wilaya ya Siha wamekuwa mabingwa wa Mpira wa Wavu kwa wasichana
ii)
Wilaya ya Siha wamekuwa pia mabingwa wa Mkoa wa Kilimanjaro katika
mchezo wa Kikapu kwa Wasichana
iii)
Wilaya ya Siha pia imechukua nafasi ya kwanza kwa mchezo wa riadha
mita 3000 ambapo mkimbiaji wa Siha alivunja rekodi ya mkoa kwa kukimbia kwa
kasi zaidi kuliko wakimbiaji wote walioshiriki mwaka 2017
iv)
Wilaya ya Siha pia ilipata nafasi ya pili kwa mchezo wa wavu kwa Wavulana
Aidha, Wilaya ya Siha imefanikiwa kutoa
wachezaji 10 wanaounda timu ya Mkoa wa Kilimanjaro itakayoweka kambi yake kwa
ajili ya kushiriki mashindano ya Taifa ya umoja wa michezo kwa shule za sekondari
(UMISSETA 2017)
No comments:
Post a Comment