Wednesday 31 May 2017

Wilaya ya Siha yang'ara michezo UMISSETA Mkoa wa Kilimanjaro





Siha yang’ara michezo ya UMISSETA Mkoa wa Kilimanjaro
Timu ya Michezo ya wanafunzi wa shule za sekondari Wilaya ya Siha imekuwa tishio kwa michezo mbalimbali kwa mkoa wa Kilimanjaro iliyomalizika hivi karibuni mjini Moshi.

Katika michezo hiyo Timu ya  Wilaya ya Siha imefanikiwa kutangazwa mabingwa wa Mkoa wa Kilimanjaro katika michezo ifuatayo:-
i)                  Wilaya ya Siha wamekuwa mabingwa wa Mpira wa Wavu kwa wasichana
ii)                Wilaya ya Siha wamekuwa pia mabingwa wa Mkoa wa Kilimanjaro katika  mchezo wa Kikapu kwa Wasichana  
iii)             Wilaya ya Siha pia imechukua nafasi ya kwanza kwa mchezo wa riadha mita 3000 ambapo mkimbiaji wa Siha alivunja rekodi ya mkoa kwa kukimbia kwa kasi zaidi kuliko wakimbiaji wote walioshiriki mwaka 2017
iv)             Wilaya ya Siha pia ilipata nafasi ya pili kwa mchezo wa wavu kwa Wavulana

Aidha, Wilaya ya Siha imefanikiwa kutoa wachezaji 10 wanaounda timu ya Mkoa wa Kilimanjaro itakayoweka kambi yake kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Taifa   ya umoja wa michezo kwa shule za sekondari (UMISSETA 2017)

No comments:

Post a Comment