Friday 12 October 2018

UJENZI WA BARABARA LAMI SANYA JUU-ELERAI

Wajumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Kilimanjaro pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Siha na uongozi wa Chama cha Mapinduzi Siha wakikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya lami Sanya Juu hadi Elerai km 32.2










kazi ya ujenzi ikiendelea katika eneo la Dartch Kona karibu na Makao makuu ya Halmashauri ya Siha 



Mhe. Godwin Mollel Mbunge wa Jimbo la Siha akishiriki katika ukaguzi wa barabara hiyo eneo la Kata ya Ngarenairobi


wajumbe wa kamati ya Siasa ya mkoa wa Kilimanjaro na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Siha wakishiriki katika kukagua kazi ya ujenzi wa barabara hiyo eneo la Ngarenairobi


Mbunge wa jimbo la Siha mhe.Godwin Mollel (kulia) akikagua ujenzi huo eneo la Ngarenairobi West Kilimanjaro




Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa KILIMANJARO mhe BOY SAFI akitoa maelekezo ya juu ya ujenzi wa barabara hiyo  akiwa katika ofisi za mkandarasi GEO ENGENEERING CHINA  

Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Onesmo Buswelu (aliyevaa kofia) akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro kabla ya kuanza ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya lami km 32.2 Sanya Juu hadi Elerai 



Mhe Onesmo Buswelu(katikati aliyevaa kofia)  Mkuu wa Wilaya ya Siha akitoa maelezo kwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara ya lami Siha 

muonekano wa barabara inayojengwa eneo la Dartch kona karibu na makao makuu ya Halmashauri ya Siha



Tuesday 9 October 2018

HABARI ZA MATUKIO KATIKA PICHA

VIJANA WA CHIPUKIZI WILAYA YA SIHA WAKITOA SALAMU ZA UTII KATIKA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU SIHA TAREHE 29.09.2018

KARIBU SIHA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU TANZANIA NDG CHARLES FRANCIS KABEHO

MKUU WA WILAYA YA SIHA MHE ONESMO BUSWELU(KULIA) AKIPONGEZANA NA MKUU WA WILAYA YA HAI MARA BAADA YA MAKABIDHIANO YA MWENGE WA UHURU ,TUKIO LIMEFANYIKA KATIKA KIJIJI CHA LAWATE TAREHE 29.09.2018




MOJA YA TAARIFA ZA MIRADI YA MAENDELEO ALIYOKABIDHIWA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA NDG CHARLES FRANCIS KABEHO

VIJIJI VYOTE WILAYANI SIHA VYAPATIWA UMEME


ASILIMIA 100 VIJIJI WILAYANI   SIHA VINA UMEME
Wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro imefanikiwa kuvipatia vijiji vyake vyote 60 nishati ya umeme (ambayo ni sawa na asilimia 100) na hivyo kuongeza kasi ya wananchi kujiendeleza kiuchumi katika sekta mbalimbali.
Hayo yametolewa   na ndg Ismael Salum Meneja wa Shirika la Umeme Wilaya ya Siha tarehe 08/09/2018 katika kikao cha kamati ya ushauri ya Wilaya ya Siha, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha.

Kikao hicho chini ya Mwenyekiti Mhe. Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Siha walitoa pongezi nyingi kwa uongozi wa shirika hilo Wilaya ya Siha kwa huduma bora wanazoendelea kuzitoa kwa wananchi.

Meneja wa shirika la umeme Wilaya ya Siha alieleza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa maeneo yote katika Wilaya ya Siha yanakuwa na huduma ya umeme ili kuwezesha mpango wa Serikali ya Viwanda.

Wilaya ya Siha imefanikiwa kusambaza umeme kwa vijiji 60 kati ya 60 vilivyopo na hadi mwezi septemba, 2018 vitongoji 126 kati ya 169 vimepatiwa  huduma ya umeme.



AJIRA MPYA KADA YA AFYA HIZI HAPA


PATA NAFASI ZA KAZI AJIRA KADA YA AFYA TUMIA LINK :http://www.tamisemi.go.tz/announcement/ajira-mpya-kwa-kada-ya-afya-awamu-ya-pili

MAPOKEZI YA MWENGE SIHA TAREHE 29.09.2018

DC SIHA MHE.ONESMO BUSWELU AKIMPOKEA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA NDG CHARLES KABEHO



MBUNGE WA JIMBO LA SIHA MHE.DKT.GODWIN MOLLEL AKITOA SHUKRANI KWA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE ALIPOKUWA WILAYA YA SIHA 29.09.2018



MASISTA WA ST.HILDEGARD WAKIPOKEA MWENGE WA UHURU ULIPOTEMBELEA ZAHANATI YA ST.HILDEGARD KILICHOPO KIJIJI CHA NDINYIKA


MKURUGENZI MTENDAJI H.W SIHA VALERIAN JUWAL AKIPOKEA MWENGE WA UHURU ULIPOWASILI WILAYA YA SIHA TAREHE 29.09.2018



MKUU WA WILAYA YA SIHA MHE.ONESMO BUSWELU AKIMKABIDHI MWENGE WA UHURU MKUU WA WILAYA YA ROMBO 

SIHA YAPOKEA MIL 500 UJENZI HOSPITAL YA WILAYA


Siha yapokea Mil 500 ujenzi Hospital ya Wilaya

Serikali ya Tanzania inayoongozwa na  Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika hospital ya Wilaya ya Siha.

Mkurugenzi Mtendajji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha Ndg, Valerian Juwal aliyasema hayo katika kikao cha kamati ya ushauri ya Wilaya ya Siha kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Siha tarehe 08/10/2018.

Aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho kuwa, kupatikana kwa fedha hizo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha miundombinu ya majengo katika hospital  ya Wilaya ya Siha, ambapo zaidi wa wakazi 120,000 wa Wilaya ya Siha  wanapata huduma za afya katika Hospital ya Wilaya.

“Napenda kumshukuru Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi anavyoendelea kuwaletea wananchi wa Wilaya ya Siha fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya  maendeleo ikiwemo miradi ya Maji,Elimu,Afya,miundombinu ya barabara” alisema Juwal.