Tuesday 16 May 2017

Waliochukua Mashamba ya Kahawa watakiwa kuyaendeleza



Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu awataka wanaomiliki mashamba kwa ajili ya kilimo cha kahawa kuyaendeleza mashamba hayo kwa mujibu wa mikataba yao kabla ya Serikali haijawachukulia hatua za Kisheria ikiwa ni pamoja na kuyachukua mashamba hayo.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema hayo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha leo tarehe 15.5.2017 alipokuwa akiongea na Wakulima na Wamiliki ya mashamba yanayoendesha kilimo cha Kahawa Wilayani Siha.

Mhe. Onesmo Buswelu aliwataka maofisa ugani wote pamoja na vyama vya ushirika kuhakikisha kuwa vinawapatia wananchi elimu ya kutosha kuhusu utunzaji wa zao la kahawa kwani ndiyo zao la kiuchumi linaloweza kuwakomboa Wananchi katika umaskini wa kipato kama ilivyokuwa hapo miaka1960 na 1970.

Aliwataka wanunuzi binafsi kutoa bei nzuri kwa wakulima na kuacha tabia za kuwanyonya Wakulima  kwa kuwapa bei za chini ambazo kimsingi ndizo zinawakatisha tamaa ya kulima zao hilo.

Mhe. Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Siha ametoa wito kwa  Wananchi wa Siha kutumia vema mvua zinazoendelea kunyesha katika kupanda mazao ya kudumu kama vile zao la Kahawa ,Matunda na mazao mengine kwa faida ya kizazi cha sasa na baadaye.

No comments:

Post a Comment