Halmashauri ya Wilaya ya Siha Mkoa wa
Kilimanjaro inatarajia kutoa zaidi ya Shilingi milioni 36 kwa ajili ya mikopo ya Wanawake Wilayani hapa.
Jumla ya vikundi 12 vyenye wanufaika 249 vinatarajiwa kufaidika na fedha hizo zinazotolewa na Halmashauri ya
Wilaya ya Siha. Fedha zinazotolewa na
Halmashauri ya Wilaya ya Siha ni sehemu
ya ya asilimia 5 ya Mapato ya ndani ya Halmashauri.
Mwezi Agosti katika mwaka huu wa fedha 2016/2017 Halmashauri ya Wilaya ya Siha
ilitoa Mikopo kwa vikundi 10 vya Wanawake Wilayani Siha vilivyokuwa na
wanufaika 157 yenye thamani ya
Shilingi milioni 20 ambapo kila kikundi kilipatiwa mkopo wa Shilingi milioni
mbili.
Halmashauri ya Wilaya ya Siha katika
utekelezaji wa bajeti yake kila mwaka imekuwa
ikitenga asilimia 5 ya Mapato ya ndani kwa ajili ya Mikopo ya Wanawake na
asilimia 5 kwa ajili ya Vijana.
No comments:
Post a Comment