Tuesday 16 May 2017

Siha Yahitaji Walimu 54 wa Masomo ya Sayansi,Hisabati



Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro inahitaji walimu 54 wa masomo ya Hisabati na Sayansi kwa shule za Sekondari za Serikali.

Akitoa taarifa ya maendeleo ya shule kwa Mkuu wa Wilaya ya Siha,Mkuu wa shule ya Sekondari Fuka  Mwalimu Swalehe Kombo alieleza kuwa Shule yake inahitaji kubwa la walimu wa Sayansi na hasa kwa somo la  Hisabati.

Mkuu huyo wa Shule aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Halmashauri ya Wilaya ya  Siha  kwa kuwapatia mwalimu mmoja wa somo la Biolojia na Jiografia katika ajira mpya zilizotolewa na Serikali  hivi karibuni. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha Valerian Juwal alieleza kuwa  Wilaya ya Siha ilipata Walimu watatu wa masomo ya Sayansi katika ajira mpya zilizotangazwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi karibuni.

Alisema kuwa kati ya Walimu watatu wa masomo ya Sayansi na Hisabati waliopangwa Wilaya ya Siha mwalimu mmoja alipangwa shule ya Sekondar Fuka na wengine katika shule ya Sekondari Sanya Juu na shule ya Sekondari Nuru.

Hata hivyo alieleza kuwa Serikali bado itaendelea kuajiri Walimu wa masomo ya Sayansi kwa shule za Msingi na Sekondari kwani mahitaji bado ni makubwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Siha aliwataka Wananchi  na wadau wa maendeleo kuendelea kukamilisha ujenzi wa maabara kwani ndiyo suluhisho la pekee litakalosaidia kupatikana kwa wataalam wa Sayansi na Hisabati.

Wilaya ya Siha inahitaji jumla ya Walimu 54 wa Masomo ya Sayansi na Hisabati kwa shule za Sekondari za Serikali.

No comments:

Post a Comment