Tuesday 16 May 2017

Siha yaweka mkakati wa kuendeleza zao la Kahawa




Wakulima wa Wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro wameweka mikakati ya kulirudisha katika ubora wake zao la kahawa kama ilivyokuwa hapo miaka ya 1970 na mwaka 1960.

Mpango huo umewekwa na wakulima wa zao la Kahawa Wilayani Siha leo tarehe 15.5.2017 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha walipokutana na kufanya kikao cha pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Onesmo Buswelu.

Katika kikao hicho cha kazi Wakulima hao walimweleza Mkuu wa Wilaya ya Siha changamoto mbalimbali zilizosababisha kushuka kwa uzalishaji wa zao la Kahawa Wilayani Siha.Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na:-
·        Kushuka kwa bei ya kahawa kutoka kwa wanunuzi binafsi pamoja na vyama vya ushirika
·        Ukame wa muda mrefu katika Wilaya ya Siha
·        Kukosekana kwa mbegu bora ya zao la  kahawa
·        Hali ya kukata tama kwa baadhi ya wakulima na badala yake kutafuta zao mbadala
Akishiriki katika kikao hicho,Mkuu wa Wilaya ya Siha aliwataka wakulima kutokata tamaa ya bei kwani Serikali itasimamia kwa karibu kuhakikisha kuwa wakulima wanapata haki yao kulingana na bei ya soko.


No comments:

Post a Comment