Friday 12 May 2017

Siha yaboresha ongezeko la Dawa katika Zahanati na Vituo vya Afya vya Umma

Hospital ya Wilaya ya Siha imeongeza manunuzi na upatikanaji wa Dawa za binadamu kwa asilimia 85 hadi kufikia mwezi Mei ,2017 kutoka asilimia 25 mwaka 2016.

Ongezeko hili limetokana na usimamizi mzuri unaofanywa na viongozi wa Serikali katika Wilaya ya Siha hasa katika kuhakikisha kuwa Wananchi na Wakazi wa Siha wanaendelea kupata dawa na matibabu ya uhakika katika Hospital za Umma.

Taarifa ya kuongezeka kwa upatikanaji wa dawa katika Zahanati,Vituo vya Afya na Hospital ya Serikali imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Onesmo Buswelu alipokuwa akiongea na vyombo vya habari kuhusu shughuli za maendeleo zilizotekelezwa na Serikali Wilaya ya Siha tangu Oktoba ,2015 chini ya Serikali ya awamo ya tano inayoongozwa na Mhe.Dkt John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment