Wednesday 15 February 2017

Watumishi wa Umma Wilayani Siha watakiwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea

Mkuu wa Wilaya ya Siha mhe:Onesmo Buswelu amewataka watumishi wa Umma ndani ya Wilaya ya Siha kufanya kazi kwa bidii na kuachana na mtindo wa kufanya kazi kwa mazoea

Hayo yamesemwa  na Mkuu huyo wa Wilaya ya Siha leo tar 15.2.2017 wakati akijadili na kupitia utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi wa Chama Tawala alipokuwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha.

Alieleza kuwa muda wa kufanya kazi kwa mazoea Sasa umefika mwisho wake na kuwataka watumishi kubadilika na kuwatumikia wananchi na wakazi wa Siha kwa nguvu na juhudi zaidi ili kutimiza malengo yaliyowekwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alieleza kuwa ,Serikali inawategemea watumishi wa Umma kwa kuzingatia kuwa wapo katika ujuzi na maarifa mbalimbali yanayoweza kutoa huduma bora kwa JAMII na siyo bora huduma.

"Nawaombeni tena kama nilivokuwa nawataka mara zote kuwa,kila mtumishi katika idara yake aone namna gani anaweza kufanikisha utoaji wa huduma nzuri kwa maendeleo ya Siha na wakazi wake,aliongeza Mkuu wa Wilaya"

Mkuu wa Wilaya mhe. Onesmo Buswelu aliwataka pia watumishi wa Umma kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma kama misingi ya utawala bora inavyoeleza.


No comments:

Post a Comment