Thursday 23 February 2017

Picha za matukio ya ufunguzi wa madarasa matatu shule ya msingi Lemosho - Tarafa ya Siha Magharibi

 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe: Onesmo Buswelu akiwa na wanafunzi wa darasa la kwanza katika moja ya madarasa aliyoyafungua Mkuu huyo wa Wilaya ya Siha.tukio hilo limefanyika leo alasiri
 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu akimfuatilia kwa makini mwanafunzi ya darasa la kwanza akifanya moja ya mazoezi ya darasa  katika moja ya madarasa aliyoyafungua leo katika Shule ya msingi Lemosho

 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe Onesmo Buswelu akikata utepe katika madarasa matatu aliyoyazindua leo katika Shule ya msingi Lemosho Tarafa ya Siha Magharibi

 Mkuu wa Wilaya ya Siha akiongea na wananchi na jumuia ya shule ya msingi Lemosho. Mkuu huyo wa Wilaya alifungua madarasa matatu na kuagiza madarasa hayo kuanza kutumika mara moja na wanafunzi wa shule hiyo ili kupunguza msongamano wa wanafunzi  madarasani.
 Wanafunzi wa shule ya msingi Lemosho wakifurahia kufunguliwa kwa madarasa matatu ya shule hiyo,ambazo ufunguzi ulifanywa na mhe Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Siha.
 Wazazi na wanafunzi wa shule ya msingi Lemosho wakimpokea kwa Shangwe Mkuu wa Wilaya ya Siha alipofika katika Shule hiyo ili kufungua madarasa matatu mapya  ya shule hiyo.
Madarasa  matatu mapya ya shule ya msingi Lemosho yaliyofunguliwa leo na Mhe. Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Siha .madarasa haya yamejengwa kwa ushirikiano wa Serikali,nguvu za wananchi ,Wahisani na wadau wa Elimu.

No comments:

Post a Comment