Hatimaye kiwango cha ufaulu ktk halmashauri ya Wilaya ya Siha Siha kimeimarika kwa shule zake za sekondari na kupanda kwa zaidi ya nafasi 40 katika nafasi za Halmashauri hapa Nchini.
Katika matokeo ya kidato cha nne Mwaka 2015 Halmashauri ya Siha ilishika nafasi ya 80 kati ya Halmashauri 178 zilizopo hapa Nchini. Matokeo yaliyotangazwa na baraza mtihani wa kidato cha nne mwaka 2016 yanaonyesha kuwa Halmashauri ya Siha katika matokeo hayo imeshika nafasi ya 40 kati ya Halmashauri 178
Aidha,katika matokeo hayo Halmashauri ya Wilaya ya Siha imeshika nafasi ya 5 katika mkoa wa KILIMANJARO na imefanikiwa kutoa mwanafunzi aliyeingia nafasi ya wanafunzi kumi bora Tanzania.
Pamoja na Wilaya ya Siha kutoa shule moja iliyoingia katika Shule kumi duni kitaifa, kiwango cha ufaulu kwa kulinganisha na Halmashauri ,Majaji na Miji kimeongezeka na nafasi ya Halmashauri imeimarika kwa mjongeo chanya.
Halmashauri ya Siha imejipanga kuendelea kuimarisha kiwango vya ufaulu katika Shule zake za sekondari katika matokeo yajayo ya kidato cha nne na sita
No comments:
Post a Comment