Thursday 16 February 2017

Kamati ya pembejeo za Kilimo Vijiji vyote Wilayani Siha yafanya kikao kufanikisha zoezi la ugawaji wa Ruzuku mwaka 2016/2017

Katibu Tawala Wilaya ya Siha Mhe. Nicodemus Bei kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Siha akifungua kikao cha kamati ya pembejeo ya kilimo  kwa Vijiji vya Wilaya ya  Siha. Viongozi  wa kamati za vijiji ni wenyeviti na makatibu waliochaguliwa na kuidhinishwa na mikutano mikuu ya Kila kijiji Wilayani Siha. Siha inajumla ya Vijiji 60 vyenye Wajumbe 6 kwa kila kijiji  wenye majukumu ya kusimamia ugawaji wa Ruzuku za pembejeo za Kilimo





Wajumbe wa kusimamia pembejeo za Ruzuku katika vijiji 60 Wilayani Siha wakimsikiliza Katibu Tawala wa Wilaya ya Siha wakati akitoa neno la ufunguzi katika kikao cha ugawaji wa Ruzuku za Kilimo kwa mwaka 2016/2017. Kikao hicho kinaendelea katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha leo tarehe 16.2.2017

No comments:

Post a Comment