Monday 20 February 2017

Asilimia 100 ya wanafunzi waliofaulu darasa la saba 2016 wachaguliwa kuendelea na Elimu ya Sekondari Wilayani Siha-Kilimanjaro

Jumla ya wanafunzi 2264 walisajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba kati yao wavulana walikuwa 1045 na wasichana 1219 sawa na asilimia 90.1 ya walioandikishwa mwaka 2010.

Jumla ya wanafunzi 2250 walifanya mtihani wa kumaliza Elimu ya msingi Wilayani Siha mwaka 2016 katika Shule za msingi 55 zenye wanafunzi wa darasa la saba. Kati ya wanafunzi waliofanya mtihani wavulana walikuwa 1037 na Wasichana walikuwa 1213 sawa na asilimia 99.38 ya walioandikishwa kufanya mtihani huo.

Aidha,katika mtihani huo jumla ya wanafunzi 1641 kati yao wavulana 729 na wasichana 912 waliofaulu kwa kiwango cha daraja A- C ambapo ni sawa na asilimia 72.93 ya waliofanya mtihani huo.

Wanafunzi wote 1641, kati yao 729 wavulana na 912  wasichana waliofaulu walichaguliwa kujiunga na masomo ya Elimu ya Sekondari katika shule za kutwa na Bweni ndani na Nje ya Wilaya ya Siha,hii ni sawa na asilimia 100 ya waliofaulu walipata nafasi ya kuchaguliwa katika Shule za Serikali.

Wastani wa Ufaulu kwa matokeo ya Darasa la saba mwaka 2016 ni 72.93 na masomo yaliyoongoza kwa ufaulu ni pamoja na  Sayansi (80%), Maarifa ya jamii(78.5),Kiswahili (77%),Kiingereza(40.2%), na somo la mwisho kwa ufaulu ni Hisabati (39.2%)

No comments:

Post a Comment