Wednesday 15 February 2017

WANAOWAPA WANAFUNZI MIMBA SASA KUKIONA

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha Valerian Juwal amewaonya wale wote watakaowasababishia MIMBA wanafunzi katika Shule za MSINGI na sekondari Wilayani siha watachukuliwa hatua kali za kinidhamu bila kujali vyeo,nafasi zao wala mahali wanaosoma.

Mkurugenzi huyo aliyasema hayo wakati akiongea na wadau wa Elimu Wilayani siha hivi karibuni kwa lengo la kujadili maendeleo na ustawi wa Elimu katika jamii ya wanaSiha.

Alisema mbali na changamoto nyingine zilizopo ambazo kimsingi zinasababisha kudorora na kushusha kiwango cha Elimu ni tatizo la baadhi ya watu kuwarubuni watoto na kuwasababishia mimba ambazo zinawakatiza watoto hao wasiendelee na masomo.

Aliwaagiza wakuu wa Shule zote za Sekondari na walimu wakuu wa shule za msingi kuhakikisha kuwa wanawachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanaosababisha mimba kwa wanafunzi.

Aliwataka walimu hao wakuu na wakuu wa Shule Wilayani siha kushirikiana na watendaji wa vijiji na Kata ili kufanikisha agizo hilo MUHIMU kwa maendeleo ya Wilaya ya Siha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Siha aliongeza kuwa hata wazazi wataonyesha wanaungana na waalifu hao pia wachukuliwe hatua za kisheria.

Wanafunzi 16 wa shule za msingi na Sekondari Wilayani Siha  walipata mimba kwa mwaka 2016 na kusababisha wanafunzi hao kukatiza ndoto zao za maisha.

Mkurugenzi akitoa wito kwa wazazi na walezi kuunga mkono jitihada za Serikali Wilayani Siha za kuhakikisha kuwa tatizo la mimba kwa wanafunzi linapungua na hatimaye baada ya muda mfupi libakie kama historia katika Shule zetu zote za msingi na Sekondari.

No comments:

Post a Comment