Wednesday 15 February 2017

Halmashauri ya Siha yaagizwa kutoa 5% Mapato ya Ndani kwa VIJANA NA WANAWAKE

Mkuu wa Wilaya ya Siha mheshimiwa Onesmo Buswelu amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha kuhakikisha kuwa asilimia 5 ya Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Siha zinatengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake.

Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo wakati akipitia taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kipindi cha mwezi Julai 2016 hadi mwezi Desemba 2016

Alieleza kuwa Halmashauri ya Siha kama zilivyo Halmashauri nyingine hapa Nchini ni lazima ihakikishe kuwa inatekeleza agizo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutenga asilimia tano ya Mapato yake ya ndani kwa ajili ya mikopo kwa vijana na Wanawake.

Alieleza kuwa ni mategemeo yake kuona kuwa asilimia hizo tano zinatengwa na kutolewa kwa wahusika kwa wakati ili mradi tu taratibu zote zifuatwe kwa kuzingatia Sheria na miongozo ya Serikali.

Hadi kufikia mwezi Desemba mwaka 2016 zaidi ya Shilingi milioni 40 fedha za Mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Siha  zimetolewa kama mikopo kwa vijana na wanawake

No comments:

Post a Comment