Sunday 17 April 2016

CHAINSAW SASA MARUFUKU MKOA WA KILIMANJARO




Mkuu wa Mkoa wa Kiliamanjaro Mh.Said Meck Sadiki amepiga marufuku matumizi ya misumeno ya nyororo(chainsaw ) katika shughuli za mazao ya misitu bila kuwa na kibali maalum.

Mh Said Meck Sadiki alitoa maagizo hayo alipokuwa katika maadhimisho ya siku ya upandaji miti mkoa Kilimanjaro yaliyofanyika katika Wilaya ya Siha tarehe 15.4.206

Mkuu wa mkoa alisema kuwa hali ya ukataji miti katika mkoa wa Kilimanjaro bado unaendelealicha ya katazo la mkoa la kutaka miti isikatwe bila kibali maalum.

Mh mkuu wa mkoa alisema kuwa ,mkoa umegundua kuwa matumizi ya chainsaw ndiyo sababu kubwa inayosababisha uharibifu wa mazingira kwa kiasi kikubwa katika mkoa wangu.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ameagiza kuwa watu wote wanaomiliki chainsaw kuzisalimisha kwa wakuu wa wilaya na wakuu wa polisi wa wilaya kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria.

Aliwaambia wananchi kuwa baada ya zoezi la kusalimisha chainsaw kukamilika mtu yeyote atakayekutwa na chainsaw atahesabiwa kuwa ni mhalifu kama walivyo wahalifu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria.

Alibainisha kuwa ofisi yake haitakuwa na mzaha na suala hili hasa ukizingatia umuhimu wa kutunza mlima Kilimanjaro kwa manufaa ya wanakilimanjaro na Taifa kwa ujumla.

Alitoa wito kwa wananchi wa Kilimanjaro kutoa ushirikiano wa kuwabainisha wale wote wanaomiliki chainsaw kinyume na utaratibu mpya wa mkoa wa Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment