Monday 17 July 2017

Oshara yaongoza matokeo ya kidato cha sita 2017 shule za Wilaya ya Siha




Oshara yaongoza matokeo kidato cha sita 2017 Wilaya ya Siha
Shule ya sekondari Oshara iliyopo kata ya Ivaeny,Tarafa ya Siha mashariki imepata matokeo mazuri ya kidato cha sita na kuwa vinara kwa shule za Wilaya ya Siha kwa  mwaka wa pili mfululizo.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa jana na kutolewa na tovuti ya baraza la mitihani la taifa nectar,matokeo hayo yameonesha kuwa shule ya Sekondari oshara imeendelea kuwa vinara katika matokeo ya kidato cha sita Wilaya ya Siha.
Matokeo hayo ya kidato cha sita yanaonesha kuwa ufaulu wa wanafunzi shuleni hapo ni kama ifuatavyo: daraja la kwanza wanafunzi  ,daraja la pili wanafunzi   ,daraja la tatu wanafunzi  .
Katika matokeo hayo hakuna mwanafunzi aliyepata daraja la nne wala sifuri na shule imeshika nafasi ya 5 kimkoa kati ya shule 43,pia shule hiyo imeshika nafasi ya 55 Kitaifa kati ya shule 449.
Wilaya ya Siha inajumla ya shule 7 za sekondari zilizofanya mtihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2017,kati ya shule hizo shule 4 ni za Serikali na 3 za taasisi za dini.

No comments:

Post a Comment