Monday 24 July 2017

DC siha aagiza kufunguliwa kwa duka la dawa hospital ya Wilaya




Mkuu wa wilaya ya siha mkoa wa Kilimanjaro mhe Onesmo Buswelu amemwagiza mganga mkuu wa hospital ya Wilaya ya siha kuhakikisha anafungua duka la dawa katika hospital ya Wilaya ya siha haraka iwezekanavyo.

Mkuu  wa wilaya ya Siha ameyasema hayo hivi karibuni alivyokuwa katika zoezi la kufungua mfumo wa kieletroniki(GoTHOMIS) katika hospital ya wilaya ya siha.

Alieleza kuwa kuwepo kwa duka la dawa ndani ya hospital ya Wilaya kutasaidia kuboresha huduma zilizopo na kwa upande mwingine ni kutimiza agizo la Serikali  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma zilizo katika viwango vya juu.

Mhe Onesmo buswelu aliwataka wataalam wa afya kuhakikisha wanautumia vema mfumo huo katika kuboresha utoaji wa  huduma bora kwa wagonjwa wanaofika katika hospital hiyo.

Wilaya ya Siha inajumla ya vituo vya afya 5,zahanati 14 na Hospital 2 ambazo zinawahudumia zaidi ya wakazi wa Siha 116,313.

No comments:

Post a Comment