Wednesday 12 April 2017

Wananchi wa Siha Wafanya kweli ujenzi wodi ya Wazazi

 Baadhi ya sehemu ya Wananchi wa Kata ya Sanya Juu Wilaya ya Siha wakishiriki katika kuchimba msingi utakaotumika katika ujenzi wa wodi ya Wazazi katika Hospital ya Wilaya ya Siha. Zaidi y Shilingi milioni 297 zitatumika katika ujenzi wa wodi ya Kinamama,Shilingi milioni 80 wodi ya watoto na milioni 511 zitatumika katika ujenzi wa jengo la upasuaji.Kukamilika kwa ujenzi huo kutasaidia kuwapunguzia wananchi wa Siha gharama za usafiri na matibabu ya kwenda hospital ya Mawenzi na KCMC mjini Moshi.

 Wananchi wa Kata ya Sanya Juu Wilayani Siha wakishiriki katika nguvu kazi za kuanza kwa ujenzi wa wodi ya Wazazi katika Hospital ya Wilaya ya Siha.tukio hili limefanyika hivi karibuni ambapo viongozi mbalimbali walishirikiana na Wananchi katika kazi za kujitolea
Wananchi wakiendele na kazi za kuandaa msingi wa ujenzi wa wodi ya Kinamama

Monday 10 April 2017

Picha za mafunzo ya manunuzi ya Umma kwa Wakuu wa shule za sekondari na Wenyeviti wa bodi za Shule Wilaya ya Siha

 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu(wa kwanza kushoto) akishiriki katika mafunzo yanayohusu manunuzi ya Umma yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha leo jumanne tarehe 10.4.2017
 Kaimu Mkurugenzi wa bodi ya manunuzi ya Umma Tanzania mhe.Godfrey Mbanyi akitoa mafunzo ya masuala ya manunuzi ya Umma kwa wahasibu wa Halmashauri,wakuu wa shule za sekondari Siha na Wenyeviti wa bodi za shule za sekondari Wilaya ya siha.
Baadhi ya wajumbe wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha wakisikiliza mafunzo ya masuala ya manunuzi ya Umma

Tuesday 4 April 2017

Picha za matukio ya jinsi Wananchi wa Wilaya ya Siha walivyoshiriki katika kuanza kwa ujenzi ya wodi ya Kinamama

 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu akishiriki ktk uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi ya wodi ya kinamama.zoezi hilo limefanyika leo humans tarehe 4.4.2017  ktk hospital ya Wilaya ya Siha na Kuhudhuriwa na Wananchi wengi wa Kata ya Sanya Juu.
 Baadhi ya kinamama wakishiriki katika kazi za uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi huo
 Mhe.Juma Jani Diwani wa Kata ya Sanya Juu akishiriki katika kazi ya ujenzi ya wodi hiyo mapema Leo jumanne tarehe 4.4.2017

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Siha Mhe.Frank Tarimo akishiriki vema katika kazi za uchimbaji wa msingi mapema Leo asbh katika eneo inapojengwa wodi ya Kinamama
 Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Onesmo Buswelu(aliyeshika kipaza sauti) akiwashukuru wananchi waliofika na kushiriki katika hatua za awali za kuchimba msingi wa wodi ya Kinamama iliyoanzwa kujengwa.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi ,Ujenzi na Mazingira Halmashauri ya Siha Mhe.Robert Mrisho akishiriki katika shughuli za kazi zilizokuwa zinendelea katika viwanja vya Hospital ya Wilaya ya Siha
 Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu ,Afya na Maji Mhe.Witson Nkini akimwagilia maji mti alioupanda karibu na eneo inapojengwa wodi ya Kinamama


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha  Valerian Juwal akishiriki katika kazi za mikono za kuchimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya Kinamama.kazi hiyo imefanyika mapema leo jumanne tarehe 4.4.2017 katika eneo la Hospital ya Wilaya lililopo Kata ya Sanya Juu Wilayani Siha