Wednesday 6 September 2017

Wanafunzi 2304 kuhitimu elimu ya msingi Wilaya ya Siha 2017





Jumla ya Wanafunzi 2304 wanatarajiwa kumaliza elimu ya msingi katika shule mbalimbali za msingi Halmashauri ya Wilaya ya Siha kwa mwaka 2017. Kati ya wanafunzi hao wavulana ni 1137 na wasichana ni 1167.

Wanafunzi hao wanatarajiwa kufanya  mitihani hiyo ya taifa ya kuhitimu masomo ya shule za msingi  kwa muda wa siku mbili tarehe 6/09/2017 na tarehe 07/09/2017.

Mitihani hiyo ya taifa itafanyika katika vituo 55 vilivyopangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Siha, kati ya vituo hivyo 52 ni shule za Serikali  ambao watafanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili na vituo 3 binafsi na Taasisi za Kidini ambazo ni English Medium .