Friday 21 July 2017

DC siha atoa siku saba hospital ya Wilaya kufunga generator hospital ya Wilaya ya Siha




Mkuu wa wilaya ya siha mhe. Onesmo Buswelu ametoa siku saba kwa mganga mkuu wa hospital ya wilaya ya siha kufunga generator katika hospital hiyo.

Hayo ameyasema tarehe 20.7.2017 katika hospital ya Wilaya ya Siha iliyopo eneo la Sanya Juu ,wakati akizindua mfumo wa kieletroniki kwa ajili ya kukusanya na uboreshaji wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa katika hospital ya wilaya.

Mkuu wa Wilaya aliwataka waganga na wauguzi kufanya kazi kwa juhudi zaidi ili kutimiza lengo la serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya kuwapatia wananchi huduma bora za afya na siyo bora huduma.

Alieleza kuwa yeye kama mkuu wa wilaya ataufuatilia utendaji kazi wa mfumo huo ili kuona kama wataalam wanautumia ipasavyo katika kuongeza huduma kwa wananchi na kuboresha ukusanyaji wa mapato kwa sehemu nyingine.

Awali mkuu wa Wilaya ya Siha alimpongeza mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha kwa kugharamia ufungaji wa mfumo huo kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri na kutekeleza agizo la Serikali  kuwa kila hospital ya wilaya kufunga mfumo wa kieletroniki kwa ajili ya ukusanyaji wa kumbukumbu na utoaji wa huduma.

Awali,mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Siha Valerian Juwal alieleza kuwa Halmashauri ya Siha itaendelea kutekeleza na kusimamia mfumo huo kwa karibu ili kuhakikisha kuwa unaleta tija kwa manufaa ya wananchi na serikali kwa ujumla.

Halmashauri ya Wilaya ya Siha imetumia jumla ya  fedha za Kitanzania Shilingi 15,642,000 ambazo ni mapato ya ndani katika kukamilisha ufungaji wa mfumo huo katika hospital ya Wilaya ya Siha

No comments:

Post a Comment