Wednesday 15 March 2017

Watendaji wa vijiji na kata Wilayani Siha wapata mafunzo elekezi ya kuboresha kazi za Umma

 Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Siha Valerian Juwal  akifungua mafunzo elekezi kwa watendaji wa Kata na Vijiji Halmashauri ya Siha.mafunzo hayo yanafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha kwa muda wa siku mbili tarehe 15.3.2017 hadi tarehe 16.3.2017
Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo watendaji wa Kata na Vijiji vyote Siha ili kuboresha utendaji wa kazi kwa kuzingatia Sheria ,taratibu na kanuni za utumishi wa Umma.
 Afisa wa Serikali za mitaa mkoa wa Kilimanjaro  Grace Makiluli akiendelea kutoa mada ya utendaji wa kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma.watumishi wa umma wametakiwa kutunza siri na Habari za Serikali ovyo ovyo bila kufuata maadili na taratibu za Umma. Katika ngazi ya Halmashauri Mkurugenzi mtendaji ndiye msemaji wa Halmashauri na ngazi ya Wilaya mhe. Mkuu wa Wilaya ndiye msemaji Mkuu kwa ngazi ya Wilaya
Washiriki wa mafunzo hayo wakisikiliza maelekezo kutoka kwa afisa utumishi na Utawala wa Halmashauri ya Siha kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha muda huu

No comments:

Post a Comment