Friday 17 March 2017

Waheshimiwa Madiwani Siha wapata mafunzo ya uongozi na utawala bora

Halmashauri ya wilaya ya Siha yawapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Siha kuhusu masuala ya uongozi,maadili na utawala bora.
Picha za matukio zimeoneshwa hapo chini

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha Valerian Juwal akifungua mafunzo ya siku moja kwa waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Siha.mafunzo hayo ya siku moja yamefanyika leo tar 17.3.2017 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha
 Afisa wa Serikali za Mitaa mkoa wa Kilimanjaro Grace Makiluli akitoa mada katika mafunzo ya siku moja ya waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Siha
 Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Siha wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha wakisikiliza kwa makini moja ya mada zilizokuwa zinatolewa

No comments:

Post a Comment