Monday 5 June 2017

Watumishi wa Umma Siha waendelea na Uhakiki




ZOEZI LA UHAKIKI KWA WATUMISHI WA UMMA- SIHA
Zoezi la uhakiki wa akaunti za mishahara kwa Watumishi wa Umma Wilayani Siha limefikia siku ya tatu leo tangu lilipoanza  siku ya ijumaa tarehe 02 Juni,2017. Zoezi hili linafanyika katika  Ofisi za Makao makuu ya  Halmashauri ya  Wilaya ya Siha. 

Hadi sasa zoezi  linaendelea kwa mafanikio makubwa hasa baada ya Watumishi wengi wa Umma katika kada mbalimbali kuonekana wakiendelea na kazi kukagua majina yao na kuhakiki kama yanaendana majina yaliyopo katika orodha ya mishahara(payroll).

Zoezi la Uhakiki kwa Watumishi wa Umma katika Wilaya ya Siha linategemewa kumalizika tarehe 06 Juni, 2017.

No comments:

Post a Comment