Monday 19 June 2017

DC Siha apiga Marufuku Biashara ya Mahindi Mabichi



Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. onesmo Buswelu amepiga marufuku biashara ya uchomaji,uuzaji na usafirishaji wa mahindi mabichi ndani na Nje ya Wilaya.

Agizo hilo amelitoa leo tarehe 19.06.2017 alipokuwa katika ukaguzi wa ujenzi wa shule mpya ya Msingi inayojengwa katika kijiji cha  Sanya hoyee Kata ya Sanya Juu.

Mkuu wa Wilaya ya Siha ameeleza kuwa sababu kubwa ya kutoa amri hiyo halali ni pamoja na malalamiko mengi aliyoyapokea ya wizi wa mahindi mabichi mashambani kutoka kwa viongozi wa Vijiji na Vitongoji Wilayani hapa.

Alieleza kuwa amri hiyo inatekelezwa kuanzia leo tarehe 19.06.2017 hadi msimu wa mavuno ya  masika kwa mwaka 2017 utakapokamilika. 

Mhe Onesmo Buswelu ametoa wito kwa Wananchi wa Siha kuhakikisha wanaweka akiba na ziada ya chakula kwa ajili ya familia zao na kuepukana na kuuza chakula chote kwa tamaa za kujipatia fedha.

amewataka pia Wananchi wa Wilaya ya Siha kuzingatia agizo la kutotumia nafaka ya mahindi kwa ajili ya utengenezaji wa pombe za kienyezi na badala yake watumia nafaka mbadala kama vile ngano na shairi kama wakiona ni lazima kufanya hivyo.

Kwa msimu wa mwaka 2017,Wilaya ya Siha inategemea kupata msimu mzuri wa chakula hasa zao la mahindi ,viazi na ndizi.

No comments:

Post a Comment