Sunday 11 June 2017

Chanjo ya Kichaa cha Mbwa kuanza kutolewa Hospital ya Wilaya



OFISI YA RAIS TAMISEMI
HALMASHAURI YA WILAYA YA SIHA

TAARIFA KWA UMMA
Mganga Mkuu wa Hospital ya Wilaya ya Siha anawatangazia Wananchi wote Wilayani Siha kuwa, Chanjo ya Kichaa cha Mbwa sasa inapatikana katika hospital ya Wilaya ya Siha kwa bei nafuu kabisa ya Shilingi elfu 30 tu.

Hivyo kwa wale wote watakaopata matatizo ya kung’atwa/kuumwa na Mbwa  wafike hospital ya Wilaya ya Siha na watapatiwa matibabu mara moja.

Aidha,kupatikana kwa huduma hii muhimu kutawasaidia Wananchi wa Wilaya ya Siha kuepukana na usumbufu wa kuwapeleka wagonjwa wao katika hospital ya Mkoa wa Kilimanjaro Mawenzi ,ambapo huduma hizi zilikuwa zinapatika hapo awali.

Wananchi na Wakazi wa Wilaya ya Siha mnaombwa kutumia fursa hii muhimu ya matibabu ili kuokoa maisha ya ndugu, jamaa na marafiki zetu wanaopatwa na janga la kung’atwa na Mbwa.

Matibabu ya Chanjo ya kichaa cha Mbwa yanatolewa kwa binadamu aliyeng’atwa na Mbwa matibabu yanapatikana muda wowote  katika Hospital yetu ya Wilaya ya Siha.

Hata hivyo,Halmashauri ya Wilaya ya Siha inatoa wito kwa Wananchi na Wakazi wa Wilaya ya Siha kufungia Mbwa  nyakati za mchana ili kuzuia  madhara kwa binadamu.

Tunawashukuru Wananchi kwa ushirikiano wetu wa dhati, tunaomba upatapo taarifa hizi umjulishe na mwenzako.

Limetolewa na:-

Kitengo cha Habari na Mawasiliano (W) Siha
Juni 09,2017

No comments:

Post a Comment