Monday 12 June 2017

Siha kuazimisha Siku ya watu wenye Ualbino tarehe 15 Juni,2017



Wilaya ya Siha kuazimisha siku ya watu wenye Ualbino
Halmashauri ya Wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro itaazimisha siku ya watu wenye Ualbino(Albinism)  siku ya Alhamis  tarehe 15 Juni,2017.

Maazimisho ya siku ya watu wenye Ualbino  Kiwilaya yanategemewa kufanyika katika ofisi ya kijiji cha Lawate huku kauli mbiu ya mwaka  2017 ikiwa “Umuhimu wa takwimu na tafiti kwa ustawi wa  watu wenye Ualbino”.

Aidha,maazimisho hayo yatafanyika kwa mara ya kwanza Wilayani Siha kwa mwaka 2017, huku Wilaya ya Siha ikiwa na historia nzuri ya kuwatunza na kuwalinda watu wenye Ualbino.
Hadi sasa Wilaya ya Siha haina tukio lolote lililotokea na kuripotiwa juu ya kitendo chochote cha kuwanyanyasa,kuwajeruhi au mauaji ya walemavu wa ngozi waliopo katika Wilaya ya Siha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha anatoa wito kwa Wananchi na Wakazi wa Wilaya ya Siha kuendelea na moyo huo wa upendo wa kuwatunza na kuwalinda ndugu zetu wenye Ualbino hasa kwa kuwapatia mahitaji yao muhimu kama elimu,huduma za Afya na huduma nyingine muhimu.

Wilaya ya Siha inakadiriwa kuwa na watu wenye Ualbino wapatao 11 ambao wanaishi na jamii katika maeneo tofauti tofauti Wilayani hapa.


No comments:

Post a Comment