Wednesday 2 April 2014

NMB YAINGIA SIHA RASMI

hatimaye Wilaya ya Siha imefanikiwa kupata huduma za kibenki baada ya banki ya NMB kufungua huduma zake katika Wilaya ya Siha

huduma hizi za kibenki zimeanza kutolewa na banki hiyo kuanzia tarehe 25.3.2014 katika mji mdogo wa sanya Juu karibu na barabara inayoelekea ofisi za Halmashauri ya Siha na pembeni mwa Kituo cha mafuta cha Kuringe Petrol station

huduma zinazotolewa na banki hiyo ni pamoja na huduma ya kuweka pesa, huduma ya kutoa pesa,huduma ya kufungua akaunti na Huduma za ATM

Wananchi wa Wilaya ya Siha wamekuwa wakikosa huduma za kibenki kwa muda mrefu sasa na hivyo kuwafanya baadhi ya wananchi kuamua kuweka fedha zao ndani ya nyumba zao au kuchimbia chini jambo ambalo limekuwa likisababisha kuhatarisha maisha yao kwa uvamiwa na watu wabaya.

wananchi wengi wa Wilaya ya siha wanaishukuru Banki ya NMB kuwa mkombozi wao kwa kuwapatia huduma za kibenki karibu na kuwatambua kuwa nao wanastahili kupata huduma hizo ili kuboresha uchumi wa  wananchi wa Siha


2 comments:

  1. NMB manjulikana kama wakombozi wa wanyonge

    ReplyDelete
  2. HII NI HABARI NJEMA KWA MAENDELEO YA WILAYA YA SIHA. AWALI WATUMISHI NA WANANCHI WENGINE WALIKUWA WANATUMIA BENKI YA WILAYA JIRANI AMBAPO MATUMIZI YA AWALI YALIFANYIKA WILAYANI HUMO NA HIVYO KUFIFISHA MAENDELEO YA SIHA.
    KWASASA MZUNGUKO WA FEDHA UTAKUWA NDANI YA WILAYA. JITIHADA ZIENDELEE ZA KUZISHAWISHI BENKI NYINGINE KUWEKEZA SIHA PIA.
    SIHA OYEEEEE!

    ReplyDelete