Sunday 6 April 2014

CCBRT WATOA HUDUMA ZAO KWA WALEMAVU SIHA



Shirika lisilo la kiserikali (CCBRT) tawi la Moshi leo limetoa huduma zake katika halmashauri ya wilaya ya siha katika Jengo jipya la Hospital ya Wilaya ya Siha lililopo karibu na mji mdogo wa sanya Juu
Shirika hilo lenye makao yake makuu Dar es salaam na lina tawi lake kubwa katika mji wa Moshi eneo la kaloleni Pasua leo limetoa huduma mbalimbali za kuwachunguza na kuwapatia matibabu na hasa ushauri kwa walezi wa walemavu ambao leo walifurika kwa wingi katika jingo hilo jipya la Hospital ya wilaya ya Siha

 Mkurugenzi wa CCBRT tawi la Moshi alisema kuwa baadhi ya huduma ambazo zinatolewa na shirika hilo kwa  watoto wenye umri chini ya miaka 18 na wanawake  ni pamoja na watoto  wenye matatizo ya Mpasuko wa mdomo(cleft Lip),Kuvuja mkojo kwa wanawake baada ya kujifungua(VVF),miguu iliyopinda kwenye nyayo 

Ruth Mlay mkurugenzi wa CCBRT-Moshi aliongeza kuwa mbali na huduma hizo pia wanatoa huduma kwa watoto wenye mtindio wa ubongo(cerebral Palsy),watoto wenye uvimbe Mgongoni(spina Bifida) na pia watoto wenye kichwa kikubwa (Hydrochephalus)
Akiongea katika shughuli hiyo  Daktari Mkuu wa Wilaya ya Siha Dr Best Magoma alisema kuwa jambo la kwanza walilolifanya ni kuwagundua walemavu wote katika Wilaya ya siha na maeneo wanayotoka. Alisema kuwa anawashukuru Wananchi wote wa Siha kwa kuitikia wito na kutoa ushirikiano wa kutosha hadi zoezi hili zimefankiwa kwa kiasi kikubwa

Pia Dr Best magoma aliwashukuru viongozi wa taasisi mbalimbali hasa taasisi za dini ambazo alisema zimetoa ushirikiano mkubwa sana wa kuhamasisha jamii hasa za vijijini kwa ajili ya kufanikisha kazi hii kubwa na yenye manufaa kwa jamii. Alisema kuwa Wilaya ya Siha hadi sasa inajumla ya walemavu mbalimbali wapatao 552 wenye ulemavu wa aina mbalimbali

Mkuu huyo wa Idara ya afya katika Wilaya ya Siha aliongeza kuwa walemavu wanayo haki ya kuishi na kujitegemea iwapo jamii itawajea uwezo badala ya kuwafungia ndani na kuwaona kama ni mkosi katika familia. Aliomba jamii kubadilika sasa na kuondokana na dhana potofu ya kuwatenga walemavu katika shughuli za kijamii

Afisa ustawi wa jamii ndugu Peter Msaka akiongea katika zoezi hilo alisema kuwa bado elimu zaidi inahitajika kwa jamii ili kuweza kuondokana na mila zisizo na maana za kuwatenga na kuwadharau walemavu katika jamii. Alitoa wito kwa jamii kuwa walemavu wasifichwe majumbani na badala yake  wapelekwe hospitalini mapema ili wapate matibabu

No comments:

Post a Comment