hatimaye Wilaya ya Siha imefanikiwa kupata huduma za kibenki baada ya banki ya NMB kufungua huduma zake katika Wilaya ya Siha
huduma hizi za kibenki zimeanza kutolewa na banki hiyo kuanzia tarehe 25.3.2014 katika mji mdogo wa sanya Juu karibu na barabara inayoelekea ofisi za Halmashauri ya Siha na pembeni mwa Kituo cha mafuta cha Kuringe Petrol station
huduma zinazotolewa na banki hiyo ni pamoja na huduma ya kuweka pesa, huduma ya kutoa pesa,huduma ya kufungua akaunti na Huduma za ATM
Wananchi wa Wilaya ya Siha wamekuwa wakikosa huduma za kibenki kwa muda mrefu sasa na hivyo kuwafanya baadhi ya wananchi kuamua kuweka fedha zao ndani ya nyumba zao au kuchimbia chini jambo ambalo limekuwa likisababisha kuhatarisha maisha yao kwa uvamiwa na watu wabaya.
wananchi wengi wa Wilaya ya siha wanaishukuru Banki ya NMB kuwa mkombozi wao kwa kuwapatia huduma za kibenki karibu na kuwatambua kuwa nao wanastahili kupata huduma hizo ili kuboresha uchumi wa wananchi wa Siha
Wednesday, 2 April 2014
HATIMAYE NMB YAINGIA SIHA RASMI
Banki ya NMB imefungua huduma zake katika halmashauri ya wilaya ya siha Kuanzia tarehe 25.03.2014 na kuanza kutoa huduma zake kwa Wananchi wa Wilaya ya Siha
banki hii ambayo imekuwa ya kwanza kufunguliwa katika Wilaya ya Siha tangu kuanzishwa kwa wilaya hiyo mwaka 2007. banki hii ambayo itasaidia Wananchi wa wilaya ya siha kuweza kuhifadhi fedha zao kwa usalama zaidi na kuwaepushia wananchi wa Wilaya ya Siha kero waliyokuwa wanaipata hapo mwanzoniu
huduma zinazotolewa na banki hii ambayo ipo kwa mtindo wa Mobile banki ni pamoja na K
banki hii ambayo imekuwa ya kwanza kufunguliwa katika Wilaya ya Siha tangu kuanzishwa kwa wilaya hiyo mwaka 2007. banki hii ambayo itasaidia Wananchi wa wilaya ya siha kuweza kuhifadhi fedha zao kwa usalama zaidi na kuwaepushia wananchi wa Wilaya ya Siha kero waliyokuwa wanaipata hapo mwanzoniu
huduma zinazotolewa na banki hii ambayo ipo kwa mtindo wa Mobile banki ni pamoja na K
SIHA YAANZISHA GAZETI
Halmashauri ya Wilaya ya Siha inategemea kuanzisha gazeti litakalokuwa linamilikiwa na halmashauri hiyo. lengo la kuanzishwa kwa gazeti hilo ambalo litajulikana kwa jina la SihaLeo ni pamoja na kupanua wigo wa mawasiliano ya umma ya kuwapatia habari wananchi wote wa wilaya ya siha na Mikoa ya kanda ya kaskazini kwa ujumla
Halmashauri hiyo ya Siha kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo inadhamiria kuwapatia wananchi huduma ya upashanaji wa habari ili kukuza dhana ya uwajibikaji na utawala bora katika kuwahudumia wananchi wake
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Siha ndugu Rashid Kitambulio aliyasema haya wakati aliongea na wanahabari waliomtembelea ofisini kwake juzi walipokuwa wakipata taarifa mbalimbali za utekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi ya mwaka 2010.
mkurugenzi huyo alisema kuwa hadi sasa tupo kwenye hatua mbalimbali za kuanzisha na kuzindua gazeti hilo la halmashauri. aliongeza kuwa magazeti yapo mengi lakini gazeti hili liatakuwa na tofauti kubwa kwani litashughulikia mambo ya kijamii zaidi hasa wanaoishi vijijini na maeneo ya pembezoni.
Ndugu Rashid Kitambulio ambaye pia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya Siha ,aliwataka wananchi wa mikoa ya kanda ya kaskazini kujivunia gazeti hilo kwani litakuwa kama alama ya kanda ya kaskazini kwa ajili ya kuwapatia habari na kuwaunganisha wananchi wa jamii mbalimbali wanaishi katika mikoa yote ya kanda ya kaskazini na Tanzania kwa Ujumla.
akizungumza na wanahabari hao katika ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Siha ,Afisa Uhusiano wa Halmashauri hiyo alisema kuwa kama mambo yatakewnda vizuri gazeti hilo litazinduliwa tarehe 26.04.2014 katika maadhimisho ya sherehe za Muungano yanayotegemewa kuadhimishwa Kimkoa katika Wilaya ya Siha
Ishara na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Muungano wetu wa miaka 50 ni pamoja na Halmashauri ya siha Kuwa na chombo chake cha kuwapatia wananchi taarifa mbalimbali za maendeleo na kijamii
Monday, 24 March 2014
WANANCHI SIHA WANUFAIKA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII
Shirika
lisilo la kiserikali FARM ACCESS kutoka nchini Uholanzi limeonyesha dhamira ya
dhati katika kuboresha afya ya wananchi wote wa wilaya ya siha kupitia mfuko wa
afya ya jamii(CHF).
Hayo
yalisemwa na meneja wa mradi huo ndugu Henri Maro katika moja ya mafunzo
yaliyotolewa na shirika hilo kwa watendaji mbalimbali Wilayani Siha yaliyokuwa
na malengo ya kuongeza uelewa kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko huo kwa umma
Dr.
Best Magoma Mkuu wa Idara ya Afya katika Halmashauri ya Siha kabla ya
kumkaribisha mkurugenzi mtendaji alisema kuwa mfuko wa afya ya jamii Wilayani
Siha ulianza mwaka 2012 kupitia chama cha wakulima wa kahawa KNCU.Aliongeza
kuwa hadi sasa mwaka wa 2014 mfuko una wanachama zaidi ya kaya 1400 katika
wilaya ya siha. Aliongeza kuwa huduma hizi zitatolewa katika hospital za
umma,binafsi na za mashirika ya dini pia
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Siha ndugu Rashid Kitambulio kwa upande wake aliwashukuru wawakilishi wa
shirika la FARM ACCESS Kwa kuichagua Wilaya ya siha kuwa miongoni mwa Wilaya
chache za Tanzania zilizoonyesha nia na dhamira ya kweli katika kuboresha afya
ya wananchi wake.
Katika
hotuba yake fupi mkurugenzi wa siha aliawaomba wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha
zoezi hilo lenye manufaa kwa wananchi wa kawaida hasa wale wasio na sekta rasmi
hasa waishio vijijini.
Wilaya
ya Siha imeweka malengo ya kufikia asilimia 30 ya kaya zote zilizopo wilayani
siha hadi ifikapo mwaka wa 2015. Mfuko huu wa afya ya jamii utasaidia kuboresha
afya za wananchi wa wilaya ya Siha kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na mifuko
mingine inayojali watumishi wa umma pekee.
SIHA YAPATA WALIMU ZAIDI YA 145
Halmashauri ya wilaya ya siha imepata walimu wa ajira mpya zaidi ya 145 kwa shule za msingi na sekondari kwa mwaka wa 2014
Hayo yalisemwa na wakuu wa idara za elimu msingi ndg Rose Sandi na Abraham Kanji mkuu wa idara ya elimu sekondari wote wawili walisema kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji
wilaya ya siha imejipanga vema kuwapokea walimu waliopangwa katika wilaya ya siha ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa na kuwa na mwanzo mzuri
kati ya walimu hawa waliopangwa wilaya ya siha ,walimu 113 ni wa shule za sekondari na zaidi ya walimu 34 ni wa shule za msingi. walimu hawa watasaidia kupunguza upungufu wa walimu na kuongeza ufaulu wa kitaaluma unakuwa siku hadi siku katika wilaya ya siha. wilaya ya siha ina jumla ya shule 13 za sekondari zinazomilikiwa na serikali na shule 54 za msingi zinazomilikiwa na serikali pia.
wilaya ya siha ni wilaya yenye mazingira mazuri ya kufanyia kazi na huduma zote za muhimu zinapatikana katika maeneo yote ya wilaya ya siha kama vile maji safi na salama,umeme,barabara na mawasiliano ya uhakika
Hayo yalisemwa na wakuu wa idara za elimu msingi ndg Rose Sandi na Abraham Kanji mkuu wa idara ya elimu sekondari wote wawili walisema kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji
wilaya ya siha imejipanga vema kuwapokea walimu waliopangwa katika wilaya ya siha ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa na kuwa na mwanzo mzuri
kati ya walimu hawa waliopangwa wilaya ya siha ,walimu 113 ni wa shule za sekondari na zaidi ya walimu 34 ni wa shule za msingi. walimu hawa watasaidia kupunguza upungufu wa walimu na kuongeza ufaulu wa kitaaluma unakuwa siku hadi siku katika wilaya ya siha. wilaya ya siha ina jumla ya shule 13 za sekondari zinazomilikiwa na serikali na shule 54 za msingi zinazomilikiwa na serikali pia.
wilaya ya siha ni wilaya yenye mazingira mazuri ya kufanyia kazi na huduma zote za muhimu zinapatikana katika maeneo yote ya wilaya ya siha kama vile maji safi na salama,umeme,barabara na mawasiliano ya uhakika
Subscribe to:
Posts (Atom)