Monday 24 March 2014

SIHA YAPATA WALIMU ZAIDI YA 145

Halmashauri ya wilaya ya siha imepata walimu wa ajira mpya zaidi ya 145 kwa shule za msingi na sekondari kwa mwaka wa 2014
Hayo yalisemwa na wakuu wa idara za elimu msingi ndg Rose Sandi na Abraham Kanji mkuu wa idara ya elimu sekondari wote wawili walisema kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji
wilaya ya siha imejipanga vema kuwapokea walimu waliopangwa katika wilaya ya siha ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa na kuwa na mwanzo mzuri
kati ya walimu hawa waliopangwa wilaya ya siha ,walimu 113 ni wa shule za sekondari na zaidi ya walimu 34 ni wa shule za msingi. walimu hawa watasaidia kupunguza upungufu wa walimu na kuongeza ufaulu wa kitaaluma unakuwa siku hadi siku katika wilaya ya siha. wilaya ya siha ina jumla ya shule 13 za sekondari zinazomilikiwa na serikali na shule 54 za msingi zinazomilikiwa na serikali pia.

wilaya ya siha ni wilaya yenye mazingira mazuri ya kufanyia kazi na huduma zote za muhimu zinapatikana katika maeneo yote ya wilaya ya siha kama vile maji safi na salama,umeme,barabara na mawasiliano ya uhakika

5 comments:

  1. walimu hao muwatumie vizuri kwa maendeleo ya siha na Taifa kwa ujumla

    ReplyDelete
  2. Hii inapendeza! Je kati ya hao wa sayansi wangapi?

    ReplyDelete
  3. SAFI SANA NA HONGERA SIHA
    TUNASONGA MBELE

    ReplyDelete