Monday 2 February 2015










HALMASHAURI YA WILAYA YA SIHA

 MAWASILIANO:                                        Ofisi ya Mkurugenzi        Mtendaji(W)                               TEL:  027- 2757646                                                                    S. L. P. 129,                                                           Fax:  027 2756863                                                                     Sanya Juu,
Mobile:073- 2973257                                                                  SIHA.
E-mail:dedsiha@yahoo.com




Unapojibu tafadhali taja:
Kumb Na SDC/S.10/2/VOL III/51                                                                      Tarehe 22/12/2014  











Unapojibu tafadhali taja:
Kumb Na SDC/S.10/2/VOL III/51                                                                      Tarehe 22/12/2014  

UTEKELEZAJI WA KIBALI CHA AJIRA
SIHA.

YAH: TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha anawatangazia ajira Wananchi wenye sifa za kujaza nafasi za kazi zilizo orodheshwa hapa chini watume maombi.

1. Afisa Mtendaji Kata II Nafasi 1 (TGS II)
       Sifa zinazotakiwa
·        Mwombaji awe na Elimu ya Shahada / Stashahada ya  juu katika moja ya fani ya Utawala, Rasilimali watu Sheria  Elimu ya Jamii Maendeleo ya Jamii , Usimamizi wa Fedha  Uchumi na Mipango kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali

Majukumu
·        Kusimamia Ulinzi na Usalama wa Raia na Mali zao na kuwa Mlinzi wa Amani katika Kata.
·        Katibu  wa Kamati ya Maendeleo ya Kata
·        Kuandaa Mpango Kazi wa Maendeleo ya kata na kuwasilisha kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kupitia kwa Afisa Tarafa
·        Mtendaji Mkuu wa Kata na  kiungo cha Uongozi kwa Idara zote kwenye Kata
·        Mratibu na msimamizi wa upangaji wa Mipango shirikishi na shughuli nyingine za Maendeleo katika ngazi ya Kata
·        Kuandaa na kupendekeza maoni ya kutengeneza Sheria Ndogo na kuyawasilisha katika Halmashauri za Wilaya / Miji
·        Kutafsiri na kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria , kanuni na miongozo ya Serikali katika Kata
·        Kuratibu na kuandaa taarifa za utekelezaji wa shughuli za Maendeleo katika Kata
·        Mwenyekiti wa Vikao vya Wataalamu katika ngazi ya Kata,Vijiji/ Mitaa na Asasi zisizo za Kiserikali
·        Kupokea na kutatua matatizo/ malalamiko ya Wananchi katika Kata.
2. Afisa Mtendaji Kijiji II Nafasi 11 (TGS C)
        Sifa zinazotakiwa
·        Mwombaji awe na Elimu ya Kidato cha Nne au sita aliyehitimu stashahada katika fani ya Utawala , Sheria , Elimu ya Jamii , Usimamizi wa Fedha, Maendeleo ya Jamii na Sayansi ya Jamii kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo Dodoma au Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali.

Majukumu
·        Kusimamia Ulinzi na usalama wa Raia na mali zao kuwa Mlinzi wa Amani na Msimamizi wa Utawala Bora katika Kijiji.
·        Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Kijiji.
·        Katibu wa Mikutano na Kamati zote za Halmashuri ya Kijiji
·        Kutafsiri na kusimamia Sera , Sheria na Taratibu
·        Kiongozi wa Wakuu wa Vitengo vya Kitaalam katika Kijiji
·        Kusimamia, kukusanya na kuhifadhi kumbukumbu zote za nyaraka za Kijiji
·        Kusimamia utungaji wa Sheria Ndogo za Kijiji

3. Katibu Mahsusi III Nafasi 4 (TGS B)
        Sifa zinazotakiwa
·        Waombaji  wawe na Elimu Kidato cha nne (Form IV)
·        Waombaji wawe wamehudhuria mafunzo ya uhazili na kufaulu mitihani ya hatua ya tatu
·        Waombaji wawe wamefaulu somo la Hatimkato na Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja.
·        Waombaji wawe wamepata mafunzo ya kompyuta kutoka Chuo chochote kinachotambulika na Serikali
·        Waombaji wawe wamepata cheti katika programu za windows, Microsoft office , Internet E- Mail na Publisher

Majukumu
·        Kuchapa barua , taarifa na nyaraka za kawaida
·        Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa
·        Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada , nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini
·        Kusaidi kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake  na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao
·        Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa walio sehemu alipo , na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika

4. Msaidizi wa kumbukumbu II Nafasi 2 (TGS B)
        Sifa  zinazotakiwa
·        Waombaji wawe na Elimu ya Kidato cha Nne (Form IV)
·        Waombaji wawe na cheti cha Utunzaji kumbukumbu katika mojawapo ya fani za Afya, Masijala na Mahakamani na Ardhi.
        Majukumu
·        Kutafuta kumbukumbu / nyaraka / mafaili yanayohitajiwa na wasomaji
·        Kuchambua , kuorodhesha  na kupanga ( classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya Ofisi
·        Kuweka / kupanga kumbukumbu / nyaraka katika reki ( file racks/cabinets) katika masijala / vyumba vya kuhifadhi kumbukumbu
·        Kuweka kumbukumbu ( barua , nyaraka nk) katika mafaili

5. Mchapa hati II Nafasi 1 (TGS B)
        Sifa zinazotakiwa:
·        Mwombaji awe amehitimu Kidato cha Nne au Sita
·        Mwombaji awe amefaulu Mtihani wa Uhazili hatua ya II kutoka chuo cha  Utumishi wa Umma
·        Mwombaji awe na ujuzi wa Kompyuta  Hatua ya I na II kutoka Vyuo  vinavyotambulika na Serikali
               
          Majukumu
·        Kuchapa Taarifa za uthamini na Hati za Fidia
·        Kuchapa Nyaraka na Hati za kumiliki Ardhi

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 21/01/2015.

Maombi yote yatumwe kwa :
Mkurugenzi Mtendaji, 
Halmashauri ya Wilaya ya Siha ,
S.L.P. 129,
Sanya Juu –Siha.

Limetolewa na:-




Rashid S. Kitambulio
Mkurugenzi Mtendaji (W)
SIHA.

No comments:

Post a Comment