Thursday 25 April 2019

WANANCHI SIHA MAGHARIBI WAFURAHIA BARABARA YA LAMI

Wananchi wa Tarafa ya Siha Magharibi wameendelea kupata mafanikio ya Serikali ya awamu ya tano kutokana na kuunganishwa na barabara kiwango cha lami inayotoka Sanya Juu kupitia Ngarenairobi hadi Elerai. Barabara hiyo inayotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni mara baada ya ujenzi  wake kukamilika muda wowote kuanzia sasa.
Kwa pamoja Madiwani wanaotoka katika Kata za Ngarenairobi,Ndumet na Mitimirefu wameeleza  kufurahishwa na utendaji kazi  uliotukuka wa Mhe  Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa kwa kuwajengea barabara bora na ya kisasa kwa kiwango cha Lami. 
Akielezea ujenzi huo Diwani wa Kata ya Ndumeti Mhe. Jackson Rabo amesema kuwa Wananchi wa Kata yake wanampongeza Rais Magufuli kwa jinsi alivyofanikisha ujenzi huo ambao ulishindikana katika awamu zote zilizopita lakini umewezekana katika Serikali ya  awamu hii ya tano. Sisi kama wananchi hatuna cha kumpa Mhe. Rais wetu bali tutazidi kumwombea Mungu ili azidi kumpa nguvu na maisha marefu zaidi.  
Kujengwa kwa barabara hiyo kumeanza kuongeza msafara mkubwa wa Watalii wanaopita barabara hiyo kupanda mlima  Kilimanjaro kupitia lango la Londrosi . kwa upande wa mazao ya chakula  kama vile viazi mviringo,karoti,Maharage,ngano,na aina mbalimbali za mboga yanayopatikana kwa wingi katika eneo la West Kilimanjaro na kusafirishwa katika mikoa ya Arusha,Tanga,Dar es salaam na Nchi jirani ya Kenya yanasafirshwa kwa urahisi kwa sasa kutokana na sehemu kubwa ya  ujenzi wa barabara hiyo kukamilika . 
Kujengwa kwa barabara hii kumetokana na juhudi za  Serikali ya awamu ya tano za kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo mengi ya Nchi ya Tanzania ikiwemo Wilaya ya Siha. Kwa mara ya kwanza tangu Uhuru ya Tanzania upatikane mwaka 1961 wananchi wameshuhudia kujengwa kwa barabara ya lami kutoka Sanya Juu  hadi Ngarenairobi kuelekea Elerai yenye jumla ya Kilomita 32.3 kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bil 52.3 kutoka Serikali ya Tanzania.
BARABARA YA LAMI WEST INAVYOONEKANA PICHANI HAPA CHINI
Muonekano wa barabara hiyo karibu na Makao Makuu ya Halmashauri ya Siha
Muonekano wa barabara mpya ya lami kuelekea West Kilimanjaro hapa ni eneo la karibu na barabara ya NARCO
kipande cha barabara hii kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Siha kama inavyoonekana pichani hapo juu
Ubora wa barabara hii karibu na barabara inayoelekea TALIRI

No comments:

Post a Comment