Thursday 25 April 2019

KINAPA WATOE MSAADA AJALI YA MOTO VISITATION GIRLS -SIHA

Mamlaka ya hifadhi ya mlima Kilimanjaro (KINAPA) leo tarehe 5.4.2019 wametoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Visitation kutokana na janga la moto lililotokea hivi karibuni na kuunguza vifaa mbalimbali vya wanafunzi wa shule hiyo.
Akiwasilisha msaada huo kwa Mkuu wa shule hiyo,Mwakilishi wa hifadhi ya Taifa ya mlima Kilimanjaro KINAPA ndugu Elibariki Eliangilisa alieleza kuwa KINAPA wametoa vifaa mbalimbali kwa wanafunzi wa shule hiyo  vyenye thamani ya shilingi milioni 2 ikiwa ni sehemu ya mchango wao kama wadau wakubwa wa elimu na lengo likiwa ni  kuwapa pole wanafunzi waliopoteza vifaa vyao wakati wa janga la moto.
Alieleza kuwa msaada walioutoa ni juhudi za Mhe. Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Siha ambaye aliwashirikisha kuhusu tukio la wanafunzi wa shule ya Wasichana Visitation kupoteza vifaa vyao mara baada ya tukio la moto kutokea katika bweni moja la wanafunzi,ambapo taarifa zinasemekana kuwa huenda ilitokana na hitilafu ya umeme,tunashukuru Mungu kuwa katika tukio hilo hakana madhara yoyote ya mwanafunzi kupata madhara bali ni vifaa tu ndio vilivyoteketea kwa moto.
“Naomba mpokee msaada wetu mdogo kwenu uwe kama chachu ya kuendelea kudumisha mahusiano yetu kama wahifadhi wa mlima na jamii ya watu wa Kilimanjaro” alisema Elibariki
Miongoni mwa vifaa vilivyokabidhiwa kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Visitation na Mwakilishi wa KINAPA kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ni pamoja na mashuka 100,Madaftari 150,Kalamu boksi 10, pamoja na vifaa vingine vingi vitakavyowezesha wanafunzi kujikimu


Wanafunzi wa shule ya wasichana Visitation  leo tarehe 5.4.2019 wakipokea msaada wa vifaa mbalimbali vilivyotolewa na mamlaka ya hifadhi ya mlima Kilimanjaro (KINAPA)
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Visitation wakishiriki katika kupokea vifaa mbalimbali vya msaada vilivyotolewa na mamlaka ya hifadhi ya Taifa ya mlima Kilimanjaro
wanafunzi wa shule ya wasichana Visitation wakishuhudia vifaa mbalimbali vya msaada vilikabidhiwa shuleni hapo na mwakilishi wa KINAPA

Vifaa mbalimbali vya msaada  vilivyotolewa na hifadhi ya Taifa ya mlima Kilimanjaro vikishushwa katika gari ,huku wanafunzi wa shule ya Visitation wakifurahia

No comments:

Post a Comment