Monday 17 October 2016

UTUNZAJI WA MAZINGIRA KIJIJI CHA MANIO- WILAYANI SIHA WASAIDIA WAFUGAJI WA NYUKI

Mizinga zaidi ya arobaini yakabidhiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Siha  kwa Wafugaji wa nyuki  Kijiji cha MANIO Kata ya KASHASHI WILAYA YA SIHA MKOA WA KILIMANJARO. Kata ya Kashashi pia ipo katika mpango wa utunzaji wa matumizi endelevu ya ardhi
mwakilishi wa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Siha Dr. Barnabas Mbwambo akishirikiana na Wananchi wa Kijiji cha Manio  Kata ya Kashashi katika  zoezi la utundikaji wa mizinga ya kisasa. zoezi hilo limefanyika hivi karibuni 
baadhi ya wafugaji wa Kijiji cha Manio wakisubiri kukabidhiwa mizinga katika kijiji chao
Diwani wa Kata ya Kashashi Mhe. Suzan Natai (wa tatu kutoka kulia) akipata maelezo ya kitaalamu baada  ya zoezi la kukabidhiwa mizinga ya nyuki kwa wafugaji wa kijiji cha Manio.

No comments:

Post a Comment