Monday 17 October 2016

PICHA ZA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA BABA WA TAIFA WILAYANI SIHA

Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Onesmo Buswelu akitoa hotuba yake katika maadhimisho ya kumbukumbu ya baba wa Taifa mwl Julius K Nyerere. Maadhimisho hayo yalifanyika katika uwanja wa CCM Sanya Juu tarehe 14.10.2016
Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe. Onesmo Buswelu ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika maadhimiro ya miaka 17 ya kumkumbuka baba wa taifa mwl Julius K Nyerere. Mkuu huyo wa Wilaya aliagiza fedha zote za posho zilizokuwa zimetolewa kwa watumishi wa ofisi yake na ile ya Mkurugenzi wa Halmashauri ikiwa ni pamoja na za maandalizi ya mwenge zilizokuwa zimetengwa kwa mwaka huu 2016/2017 zielekezwe kununulia madawa hospital ya Wilaya na kuboresha miundombinu Zahanati ya Ormelil.
Mmoja wa watoa mada Katika maadhimisho ya baba wa Taifa Wilayani Siha (Mwl Ngolinda wa Shule ya Sekondari Oshara) akitoa mada namna anavyomfahamu baba wa Taifa    
MKURUGENZI MTENDAJI H/W SIHA VALERIAN JUWAL (anayeshangilia kwa makofi) akifurahia maonesho yaliyokuwa yakifanywa na watoto wa Halaiki katika uwanja wa mpira wa miguu  Sanya juu. maadhimisho hayo yaliongozwa na mkuu wa Wilaya ya Siha Onesmo Buswelu(aliyevaa suti nyeusi mbele ya Bendera)
Wanafunzi wa Shule ya sekondari Sanya Juu wakitumbuiza katika maadhimisho ya kumkumbuka ya Baba wa Taifa Wilaya ya Siha.
Wanafunzi wa  Halaiki Wilayani Siha wakitoa ujumbe wa mshikamano na upendo kama ishara ya kumkumbuka baba wa Taifa Mwl Julius K Nyerere.
mmoja wa washiriki (Mzee Daniel Sandewa)  kwa niaba ya wazee wa Siha akitoa neno la Shukurani kwa Wananchi wa Siha kwa namna walivyoshiriki vema katika kumkumbuka baba wa Taifa la Tanzania

No comments:

Post a Comment