Friday, 18 September 2020

 

Mafanikio ya Halmshauri ya Siha Sekta Barabara 2015-2020

Katika kipindi cha miaka mitano Halmasauri ya Siha imepokea kiasi cha shilingi 57.2 bilioni kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati a miundombinu ya barabara kwa kiwango  cha lami,changarawe na ukarabati wa barabara vijijini.

Fedha zilizotolewa na Serikali ya Tanzania zimesaidia ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa km 32.2 kutoka Sanya Juu hadi Elerai,ujenzi wa barabara za changarawe vijijini jumla ya km 199.2.

Pia Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Dkt. John Magufuli  imewezesha Madaraja muhimu kama vile  Kisube kirisha, Lawate loiwang, Muri - Nkwamariko na Mwaru.


Aidha,Serikali ya Tanzania kupitia wakala wa Barabara TARURA imefanikiwa kufanya ukarabati wa barabara zenye urefu wa km 236.81 na kuifanya halmashauri ya Siha kuwa miongoni mwa Halmashauri hapa nchini zenye barabara zinazopitika wakati wote wa mwaka.

Mafanikio haya yote yametokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Serikali na Wananchi wa Wilaya ya Siha pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo wa ndani na nje ya Wilaya.

Wednesday, 7 August 2019

Madiwanni Siha wajifunza Kilimo & Ufugaji wa kisasa Nanenane Julai 6,2019

Madiwani wa Halmashauri ya Siha wakitembelea maonesho ya nanenane mwaka 2019 viwanja vya Njiro tarehe 6.8.2019 


 Mtaalam wa Chuo cha Nelson Mandela Arusha akielezea kuhusu matumizi sahihi ya madawa katika ukuzaji wa mazao ya chakula na biashara
 Elimu kuhusu matumizi ya maziwa kwa jamii imetolewa kwa Wah Madiwani wa Siha walipotembelea banda la Halmashauri ya Siha

 Bustani ya Siha imetia fora viwanja vya nanenane mwaka 2019
Wah. Madiwani wa Halmashauri ya Siha wakijifunza kuhusu kilimo bora ndani ya viwanja vya nanenane Arusha tarehe 6.8.2019

Friday, 12 July 2019

Pata matokeo ya Kidato cha Sita shule za Sekondari Siha mwaka 2019


Bofya hapa kuona Matokeo ya shule za Siha
http://www.sihadc.go.tz/new/angalia-matokeo-kidato-cha-sita-2019-shule-za-siha

matukio ya Mwenge wa Uhhuru wapokelewa kwa Shangwe Wilayani Siha

 Wananchi wa Kata ya Ndumeti walivyoupokea Mwenge wa Uhuru ulipowasili Wilaya ya Siha mwaka 2019


Wananchi wa Kijiji cha Matadi Kata ya Ndumeti walivyopokea Mwenge wa Uhuru katika shule ya Sekondari matadi ulipowasili shuleni hapo tarehe 20.6.2019
Kata ya Ndumeti kijiji cha Matadi  ilivyotia fora katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2019  









Madiwani Siha wapanga mkakati wa kuimarisha mapato ya ndani ya Halmashauri


Baraza la Madiwani Halmashauri ya Siha wakisikiliza Mawasilisho  ya miradi mkakati inayotarajiwa kutekelezwa katika Halmashauri ya Siha -Kilimanjaro

 Mkuu wa Wilaya ya Siha mhe. Onesmo Buswelu akiongea na Waheshimiwa Madiwani walipokuwa katika mkutano wa kawaida wa baraza tarehe 11.7.2019
Waheshimu Madiwani wa Halmashauri ya Siha wakiwa katika mkutano wa Kawaida wa Baraza la Madiwani Siha tarehe 11.7.2019 

Mkuu wa Wilaya ya Siha mhe.Onesmo Buswelu akisema jambo katika Baraza la Madiwani Halmashauri ya Siha tarehe 11.7.2019

ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Wilaya ya Siha tarehe.7.7.2019

 Mkuu wa Wilaya ya Siha mhe Onesmo Buswelu akimpokea Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi Siha tarehe 7.7.2019
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Siha mhe. Godson Ngomuo akimpokea katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa 

 Katibu Tawala wa Wilaya ya Siha Joseph Mabiti akisalimiana na katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa 

 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa ndugu Bashiru Ally akisalimiana na Wakuu wa Idara na Vitengo alipowasili katika Hospitali ya Wilaya ya Siha

 Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Siha Dkt. Barnabas Mbwambo akisalimiana na Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa
 Mbunge wa Jimbo la Siha Mhe. Godwin Mollel (katikati ) akipokea burudani kutoka ngoma za kabila la Kimaasai walipompokea katibu mkuu wa CCM Taifa
Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi Bashiru Ally akifurahia ngoma ya kimaasai alipowasili katika Hospital ya Wilaya ya Siha

Monday, 13 May 2019

WATUMISHI WANAMICHEZO SIHA WAFANYA ZIARA HIFADHI YA NGORONGORO



Timu ya mpira wa miguu ya watumishi wa Umma ikijiandaa na mchezo wa Bonanza
tarehe 4/5/2019 kati ya timu himu na Serena Hotel Timu

 Wachezaji wa Siha wakipeana mbinu za mchezo wakati wa mapumziko
Kikosi kamili cha watumishi wa Siha kilichosafiri kwenda kwenye Bonanza la michezo hifadhi ya Ngorongoro kuanzia tarehe 3/5/2019 hadi tarehe 5/5/2019
Mazoezi kabla ya mchezo ndiyo njia bora ya kuweka miili katika hali bora zaidi,timu ya Siha hapo juu ikijifua kabla ya mchezo wa Bonanza