Wilaya ya Siha inategemea kutoa chanjo ya minyoo kwa watoto zaidi ya 24000 kwa mwaka 2016.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha Rashid Kitambulio amewataka wananchi na wakazi wote wa Siha kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya watoto wetu na Taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi amewataka wazazi kuhakikisha kuwa watoto wote wenye umri wa miaka 4 hadi 14 wanapatiwa chanjo hiyo muhimu kwa ajili ya minyoo. alieleza kuwa wataalam wa afya kwa kushirikiana na Walimu watahakikisha wanasimamia zoezi hilo kwa ukamilifu ili kutimiza malengo ya kuwachanya watoto wote katika Wilaya ya Siha.
alitoa wito kwa wazazi kushirikiana na watoa huduma ili kila mtoto anayestahili apatiwe chanjo kwa wakati. Aliongeza kuwa chanjo hiyo inatolewa bure bila malipo yoyote na kuwatoa hofu wazazi wanafikiri kuwa watatakiwa kufanya malipo.
Hata hivyo mkurugenzi wa Halmashauri ya Siha alieleza kuwa matayarisho ya vifaa vyote vinavyotakiwa vimekamilika na zoezi limeanza leo tarehe 11.05.2016 katika kata zote 17 zilizopo Wilayani Siha. Alisema kuwa zoezi hilo litaendelea tarehe 12 na 13 kama halitakamilika kwa siku moja lengo ni kuhakikisha kuwa walengwa wote wanapata huduma.
Wednesday, 11 May 2016
Tuesday, 3 May 2016
mkutano wa Baraza la Madiwani Tarehe 6.5.2016
TANGAZO
MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIHA ANAWATANGAZIA WANANCHI WOTE KUWA MKUTANO WA KAWAIDA WA BARAZA LA MADIWANI KWA KIPINDI CHA ROBO YA TATU (JANUARI HADI MACHI ,2016) UTAFANYIKA TAREHE 6.5.2016 SAA 4:00 ASUBUHI.
MKUTANO HUO UTAFANYIKA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIHA.
WOTE MNAKARIBISHWA
limetolewa na Kitengo cha habari na Mawasiliano (W) SIHA
tarehe 03 Machi,2016
VIKUNDI VYA MAZINGIRA SIHA VYAJITOLEA KUPANDA MITI ZAIDI YA 10,000
baadhiya vikundi vya mazingira Wilaya ya Siha wakipanda miti eneo la makao makuu ya Halmashauri hivikaribuni
RC KILIMANJARO APONGEZA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MSITU WA WEST KILIMANJARO
Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro Mh. Said Meck Sadiki akiwa ndani ya hifadhi ya mlimaKilimanjaro eneo la Londros gate Wilayani Siha na kukagua uhifadhi wa mazingira
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,uongozi wa Wilaya ya Siha na baadhi ya Wataalam wakiwa katika hifadhi ya Taifa ya MlimaKilimanjaro hivi karibuni katika shughuli za kukagua hifadhi hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,uongozi wa Wilaya ya Siha na baadhi ya Wataalam wakiwa katika hifadhi ya Taifa ya MlimaKilimanjaro hivi karibuni katika shughuli za kukagua hifadhi hiyo
RC KILIMANJARO AKAGUA SHAMBA LA MITI WEST KILIMANJARO WILAYANI SIHA
MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO MH.SAID MECK SADIKI AKIPEWA MAELEZO YA JINSI YA KUHAMISHA MICHE YA MITI KUTOKA KITALUNI NA KWENDA KATIKAVIRIBA.HAYO YALIFANYIKAKATIKA SHAMBA LA MITI WEST KILIMANJARO TARAFA YA SIHA MAGHARIBI
hii ni mojawapo ya bustani ya miti katika shamba la miti West Kilimanjaro iliyokaguliwa na Mkuuwa Mkoa wa Kilimanjaro mh. Said M Sadiki katika ziara fupi aliyoifanya hivi karibuni Wilayani Siha. Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kukagua shughuli za shamba hilona uhifadhi wa mazingira
hii ni mojawapo ya bustani ya miti katika shamba la miti West Kilimanjaro iliyokaguliwa na Mkuuwa Mkoa wa Kilimanjaro mh. Said M Sadiki katika ziara fupi aliyoifanya hivi karibuni Wilayani Siha. Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kukagua shughuli za shamba hilona uhifadhi wa mazingira
SIKU YA UPANDAJI MITI MKOA WA KILIMANJARO YAFANYIKA WILAYANI SIHA 2016
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. Said Meck Sadiki akishiriki maadhimisho ya upandaji miti Mkoa wa Kilimanjaro yaliyofanyika Wilayani Siha tarehe 15.4.2016 eneola makao makuu ya Halmashauri ya Siha. zaidi ya miti 10,000 ilipandwa siku hiyokatika eneo hilo
Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Siha ambaye pia ni DMO wa Wilaya ya Siha Dr. Best Magoma akishiriki katika zoezi laupandaji miti Kimkoa tarehe 15.4.2016
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Siha Mh.Frank Kisinane akishiriki katika zoezi laupandaji miti Kimkoa katika eneo la makao makuu ya Halmashauri hiyo tarehe 15.4.2016
Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Siha ambaye pia ni DMO wa Wilaya ya Siha Dr. Best Magoma akishiriki katika zoezi laupandaji miti Kimkoa tarehe 15.4.2016
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Siha Mh.Frank Kisinane akishiriki katika zoezi laupandaji miti Kimkoa katika eneo la makao makuu ya Halmashauri hiyo tarehe 15.4.2016
Subscribe to:
Posts (Atom)
















