Monday 15 January 2018

Magadini Sekondari waongoza matokeo ya Utamirifu Mkoa wa Kilimanjaro 2018



Magadini Sekondari waongoza matokeo ya ”mock”  kidato cha 6 mkoa wa Kilimanjaro 2018

Hatimaye shule ya Kata ya Magadini Sekondari Wilaya ya Siha imefanikiwa kuongoza katika matokeo ya utamirifu (Mock) katika mkoa wa Kilimanjaro kati ya shule 66 za kidato cha sita zilizofanya mtihani.

Kwa mujibu wa matokeo ya mock mkoa wa Kilimanjaro yaliyotolewa hivi karibuni,shule hiyo ya Kata imefanikiwa kuzipiku shule kongwe hapa Nchini zikiwemo shule ya Ufundi Moshi,Umbwe,Ashira,Weruweru na nyingine nyingi.

Akizungumzia matokeo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Siha Valerian Juwal aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa kazi nzuri waliyofanya ya kuiletea sifa Wilaya ya Siha na Kata ya Gararagua kwa ujumla wake.

No comments:

Post a Comment