Wednesday 31 January 2018

Siha yafanya kweli matokeo kidato cha Nne 2017



Siha yashika nafasi pili Mkoa wa Kilimanjaro  matokeo kidato cha Nne 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro imeshika nafasi ya pili kati ya Halmashauri 7 za mkoa wa Kilimanjaro matokeo kidato cha nne.

Kwa mujibu ya matokeo yaliyotolewa na tovuti ya baraza la mitihani la taifa mapema jana,Halmashauri ya Siha imepanda kutoka nafasi ya 40 kitaifa mwaka 2016  hadi nafasi ya 16 mwaka 2017.

Halmashauri ya Siha inazo jumla ya shule 18 za Sekondari kati ya hizo 13 za Serikali na shule  4 za mashirika ya dini  na shule  moja inamilikiwa na mtu binafsi.


No comments:

Post a Comment