Monday, 31 October 2016

MPANGO WA PAMOJA TUWALEE WILAYANI SIHA



Mwenyekiti wa HALMASHAURI ya SIHA Mhe. Frank Tarimo(wa tatu kutoka kushoto) akifurahia Jambo katika shughuli za Kupokea taarifa ZA mpango wa pamoja Tuwalee zilizomaliza muda wake kwa miaka mitano katika HALMASHAURI ya Wilaya ya SIHA. Mpango huu ulikuwa NA jukumu la kuwawezesha watoto WANAOISHI katika mazingira hatarishi Wilayani SIHA NA limefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Wananchi wapata elimu ya kujikinga NA ugonjwa wa TB (kifua kikuu)


Wataalam wa AFYA katika hospital ya Taifa ya kifua kikuu kibongoto Wilayani SIHA WAKITOA elimu kwa umma kwa njia ya igizo ya namna bora ya kujikinga NA ugonjwa wa TB ambao unaambukiza kwa njia ya Hewa. Igizo hilo lilifanyika mbele ya mgeni rasmi mhe. Hamis Kigwangalla Naibu waziri wa AFYA,maendeleo ya JAMII,jinsia,Wazee NA watoto alipokuwa hospitalini hapo hivi karibuni ktk zoezi la kuzindua bodi ya hospital hiyo longer hapa Nchini.

Vitalu bora vya MICHE ya miti Shamba la miti West Kilimanjaro


Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya SIHA wakiangalia jinsi wataalam wa utunzaji wa MICHE ya miti katika Shamba la miti West KILIMANJARO wanavyofanya kazi hiyo

WANAFUNZI WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYANI SIHA WAKITOA UJUMBE KWA JAMII KWA NJIA YA NYIMBO

wanafunzi wa shule ya sekondari Sanya Juu wakitoa ujumbe kwa jamii kwa njia ya nyimbo katika moja ya makongamano  yaliyofanyika Wilayani Siha hivi karibuni.

vitalu vya miche ya miti shamba la miti West KILIMANJA


MICHE YA MITI KATIKA KITALU CHA MITI WEST KILIMANJARO  INAYOSUBIRIWA KUPANDWA KATIKA MVUA ZA VULI NA MASIKA

BODI YA HOSPITAL YA TAIFA YA KIFUA KIKUU YAZINDULIWA RASMI

BAADHI YA WAJUMBE WA BODI YA HOSPITAL YA TAIFA YA KIFUA KIKUU-KIBONGOTO WAKIWA NA MGENI RASMI  MHE. HAMIS KIGWANGALLA (aliyekaa mbele wa tatu kutoka kushoto)  NAIBU WAZIRI WA AFYA,MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO.

SIHA YAPOKEA MADAWATI 200 KUTOKA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA KWA AJILI YA SHULE 5 ZA MSINGI

MKUU WA WILAYA YA SIHA MHE ONESMO BUSWELU (KULIA) AKIPOKEA MADAWATI 200 KUTOKA MENEJA WA SHAMBA LA MITI WEST KILIMANJARO KWA NIABA YA WAKALA WA MISITU TANZANIA
 MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SIHA VALERIAN JUWAL (aliyevaa shati la kitenge kushoto) AKIWA NA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MWANGAZA MARA BAADA YA KUKABIDHIWA MADAWATI 30
WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI NGARENAIROBI WAKIFURAHIA MADAWATI 200 YALIYOTOLEWA NA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA .MADAWATI YALITOLEWA KWA SHULE TANO ZA MSINGI WILAYANI SIHA. NGARENAIROBI MADAWATI 50,LEMOSHO MADAWATI 50,ROSELINE MADAWATI 40,NAMWAI MADAWATI 30,MWANGAZA MADAWATI 30