Thursday 25 April 2019

WANAWAKE WILAYA YA SIHA WAPATIWA MIL 59

Halmashauri ya Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro imetoa mikopo kwa vikundi 20 vya Wanawake yenye thamani ya shilingi milioni 59
Zoezi la utoaji wa mikopo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha tarehe 16.4.2019 ambapo Kaimu mkuu wa Wilaya ya Siha mhe. Agnes Hokororo ambaye pia ni mkuu wa Wilaya ya Rombo alikuwa mgeni rasmi katika Zoezi hilo. 
Katika hotuba yake mhe. Hokororo Alitoa pongezi nyingi kwa halmashauri ya Siha kwa kupata mafanikio makubwa katika utoaji wa mikopo kwa vikundi vya Wanawake.
Napenda kuwaasa kinamama wa Wilaya ya Siha kuendelea kudumisha umoja wenu katika kuendeleza vikundi mlivyonavyo huku Serikali kupitia halmashauri itaendelea kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu alisema Mhe. Hokororo
Pia mhe. Hokororo alitoa wito kwa halmashauri ya Siha kuhakikisha kuwa,  inatoa mikopo kwa watu wenye ulemavu bila kusahau vikundi vya vijana kama ilivyo agizo la Serikali yetu.
Akizungumza kabla ya utoaji wa mikopo hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha ndugu Valerian Juwal ,alieleza kuwa mikopo inayotolewa kwa vikundi 20 vya Wanawake itawanufaisha  zaidi ya  watu 479 ndani ya Wilaya ya Siha.  Leo tunawapatia vikundi 19 kila kimoja shilingi milioni 3 na kikundi kimoja kinapata shilingi milioni 2 alisema Juwal
Alieleza kuwa kwa miaka miwili iliyopita (2016/2017 & 2017/2018) Halmashauri ya Wilaya ya  Siha imekuwa ikipata tuzo kwa kuwa miongoni mwa Halmashauri za mfano hapa Tanzania kwa kutoa mikopo kwa kiwango kikubwa.
”Napaenda kueleza kuwa katika mwaka huu wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Siha imedhamiria kushika nafasi za juu kabisa miongoni mwa Halmashauri zitakazofanikiwa kutoa mikopo kwa wingi  kwa vikundi vya  Wanawake” alisema Juwal.
Utoaji wa mikopo kwa wanawake katika Halmashauri hapa nchini ni utekelezaji wa agizo la Serikali ya awamu ya tano kuwa ,asilimia 4 za mapato ya ndani ya kila Halmashauri zitolewe kama mikopo kwa Wanawake,asilimia 4 mikopo kwa vijana na asilimia 2 itolewe kama mikopo kwa watu wenye ulemavu.
Baadhi ya Wanawake waliopatiwa mikopo wakiwa  katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Siha wakifurahia zoezi la utoaji wa mikopo

Wah. Madiwani wanawake Halmashauri ya Siha wakishuhudia zoezi la utoaji wa mikopo kwa vikundi 20 vya wanawake,zoezi lilifanyika tarehe 16.4.2019 ktk ukumbi wa Halmashauri ya Siha

Mkurugenzi Mtendaji H/W Siha ndugu Valerian Juwal (kulia) akisoma orodha ya vikundi 20  vya wanawake vilivyopatiwa mikopo ya shilingi Mil.59  na Halmashauri ya Siha 

No comments:

Post a Comment