Thursday 25 April 2019

BARABARA ZA SIHA ZABORESHWA

Wakala wa usimamizi wa barabara za mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Siha wameendelea kutekeleza azma ya Serikali ya awamu ya tano kwa vitendo kwa kuzifanyia matengenezo barabara za vijijini katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Siha.
Kwa Ujumla barabara zote katika Vijiji na Vitongoji Wilayani Siha zinapitika wakati wote na kusaidia shughuli mbalimbali za wananchi katika kusafiri na kusafirisha mazao mbalimbali ya biashara na chakula

Hii ni barabara ya Siha Sango hadi Kijiji cha Mese Wilayani Siha ikiendelea kufanyiwa matengenezo makubwa  kupitia TARURA

No comments:

Post a Comment