Thursday 25 April 2019

SANYA JUU SEKONDARI WAPEWA TUZO MCHEZO WA BASEBALL

Timu ya shule ya Sekondari Sanya Juu(Sanya Day) Kata ya Nasai  kwa mchezo wa Baseball wamepewa tuzo ya heshima baada ya kufanikiwa kushika nafasi ya pili ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa shule za Sekondari mwishoni mwa mwaka 2018.
Tuzo hiyo imetolewa na Mhe. Anna Mghwira Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro alipokuwa katika maazimisho ya juma la elimu mkoa wa Kilimanjaro lililofanyika tarehe 11.4.2019 katika uwanja wa mashujaa mjini Moshi ambapo Halmashauri zote Saba za Mkoa wa Kilimanjaro zimeshiriki kikamilifu na kuonesha mafanikio makubwa.
Katiba hotuba yake fupi ya ufunguzi wa wiki ya elimu mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Mkuu wa Mkoa alieleza kufurahishwa na mafanikio ya kitaaluma yaliyopatikana katika mkoa wa kilimanjaro kwa zaidi ya miaka mitatu sasa ambapo mkoa umeshika nafasi za juu kimasomo na kimichezo pia.
Alieleza kuwa kipekee naipongeza shule ya Sanya Juu Sekondari kwa kufanikiwa kushika nafasi ya pili Kitaifa mwaka 2018 katika mchezo wa Baseball. Nimeambiwa kuwa mwaka 2017 ndio mlikuwa mabingwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchezo huu, ambapo mlituletea heshima kubwa mkoa wa Kilimanjaro pamoja na Wilaya ya Siha
Katika utoaji wa tuzo hiyo jumla ya wanafunzi 10 na walimu wawili walioleta heshima Mkoa wa Kilimanjaro  walivalishwa nishani kila mmoja mbele ya umati mkubwa wa watu waliofurika kwa wingi katika uwanja wa mashujaa mjini Moshi.
Shule ya Sekondari Sanya Juu ipo Wilaya ya Siha na inawanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita huku wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 wakiwa wanasoma masomo ya Sayansi pekee(PCM,PCB,PGM na CBG).
wachezaji wa Timu ya Baseball Sanya Juu Sekondari wakivalishwa nishani na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ktk kilele cha juma la elimu uwanja wa mashujaa Moshi

Cheti cha Pongezi kilichotolewa kwa shule ya Sanya Juu Sekondari
Mkuu wa Shule ya Sanya Juu Mwl Elieta Kaaya akipokea cheti za pongezi kwa niaba ya timu hiyo na uongozi mzima wa shule

Wanafunzi wachezaji  wa Walimu wakifurahi mara baada ya kuitwa kuchukua zawadi zao mbele ya mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
Mwalimu wa mchezo wa Baseball Sanya juu Sec mwl Nuiya Ally akipokea zawadi yake kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

No comments:

Post a Comment