Thursday 25 April 2019

SIHA YAPATA MAFANIKIO UTOAJI ELIMU MAALUM

SIHA YAPATA MAFANIKIO ELIMU MAALUM
Halmashauri ya Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro imekuwa miongoni mwa Halmashauri za mfano katika kutoa elimu kwa watoto wenye mahitaji maalumu (watoto wenye Usonji).Hayo yamebainika katika maazimisho ya siku ya Usonji dunia ambayo kila mwaka hufanyika tarehe 2 April,,ambapo katika Wilaya ya Siha mwaka 2019 yamefanyika katika Shule ya Msingi Sanya Juu.
Katika kutekeleza uboreshaji wa elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum,Halmashauri ya Wilaya ya Siha inazo jumla ya shule 4 za msingi zinazotoa elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum(Usonji) ,shule hizo ni pamoja na Shule ya Msingi Nuru,Sanya Juu,Faraja na shule ya Msingi Naibili.
Katika shule hizo kwa mwaka huu 2019 zina jumla ya watoto 147 ambapo watoto wote wanaosoma wana mahitaji maalum(Usonji) ,Aidha walimu wenye taaluma ya kutosha na waliobobea wanafundisha shule hizo kulingana na mahitaji ya watoto husika.
Kuwepo kwa mafanikio haya kumetokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya wazazi na wadau mbalimbali wa elimu ikiwemo Serikali ya awamu ya tano ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo mdau namba moja katika kufanikisha zoezi hili muhimu la kuwapatia elimu watoto wa Kitanzania bila kujali tofauti za kijinsia,maumbile wala maeneo mtoto anapotoka.
Katika kipindi cha Serikali ya awamu ya tano (2015 hadi sasa 2019) tumeshuhudia ongezeko kubwa la wanafunzi wenye mahitaji maalum wakipelekwa mashuleni na wazazi pamoja na walezi wao, hii imetokana na Sera nzuri ya Serikali ya awamu ya Tano ya utoaji wa elimu bila malipo katika shule zote za Serikali kuanzia ngazi ya awali hadi elimu ya kidato cha nne.
Watoto wenye mahitaji maalum wakishiriki zoezi la upandaji wa Miti katika eneo la shule ya Msingi Sanya Juu tarehe 2.4.2019

Watoto wa  darasa la Nne na Tatu katika shule ya Msingi Sanya Juu wakifurahia kushiriki katika maazimisho ya siku ya Usonji Duniani tarehe 2.4.2019,ambapo Kiwilaya yalifanyika shule ya Msingi Sanya Juu.

Kupata ushauri uliotolewa kwa wazazi katika maazimisho hayo bofya 
1. Hapa

No comments:

Post a Comment