Thursday 25 April 2019

WAZAZI WATAKIWA KUWAPA ELIMU WATOTO BILA UBAGUZI-SIHA

Wananchi wa Wilaya ya Siha wameshauriwa kuwapa watoto wote elimu bila ubaguzi wa aina yoyote
Hayo yamesemwa na Mwalimu Rose Sandi  Afisa elimu shule za Msingi katika Halmashauri ya Wilayani  ya Siha  leo tarehe 2.04.2019 aliposhiriki na watoto wenye mahitaji maalumu (siku ya Usonji) katika maazimisho ya siku yao duniani.
Watoto wenye usonji wakishirikiana na wazazi wao katika zoezi la kupanda miti mapema leo katika shule ya msingi Sanya Juu
Maazimisho hayo katika Wilaya ya Siha yamefanyika katika shule ya Msingi Sanya juu na kujumuisha watoto wenye mahitaji maalumu kutoka shule mbalimbali za msingi Wilayani Siha ikiwemo shule ya Msingi  Faraja Siha .
Wanafunzi wa shule ya msingi Sanya Juu wakishiriki maazimisho ya siku ya Usonji dunia leo tarehe 2.4.2019
Katika Maazimisho hayo wazazi na jamii imetakiwa kuwapa elimu watoto wote katika familia bila   ubaguzi wa jinsia,maumbile au uwezo wa watoto katika kuelewa na kuchanganua mambo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment