Thursday 1 November 2018

WATAKAOWAPA MIMBA WANAFUNZI KUKIONA:DC SIHA


Mkuu wa Wilaya ya Siha mhe. Onesmo Buswelu ametoa onyo kali Wilayani Siha kwa watu wote wanaokatisha masomo wanafunzi wa kike kwa kuwasababishia mimba.

Hayo ameyasema katika kijiji cha Munge kata ya Donyomuruak tarehe 1/11/2018 alipokuwa akiongea na wananchi katika mkutano wa kijiji hicho uliotishwa kwa lengo la kumtambulisha mkandarasi aliyepewa kazi ya ujenzi mradi mkubwa wa   maji.

Alieleza kuwa pamoja na kumtambulisha mkandarasi leo kwa wananchi napenda kutoa onyo kali kwa watu watakaothubutu kukatisha masomo  watoto wa kike kwa kuwasababishia mimba .

“Napenda kuwaeleza kuwa kwa hili siwezi kuwa na uvumilivu lazima nitahakikisha kuwa watu wote watakaowapa mimba wanafunzi wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao” alisema Buswelu.

Mkuu huyo wa Wilaya alitoa wito kwa wananchi na wakazi wa Wilaya ya Siha kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola pamoja na viongozi mbalimbali katika jamii ili kufanikisha zoezi la kuwatafuta na kuwakamata kwa haraka watu watakaodiriki kuwapa mimba wanafunzi.


No comments:

Post a Comment