ASILIMIA
100 VIJIJI WILAYANI SIHA VINA UMEME
Wilaya
ya Siha mkoa wa Kilimanjaro imefanikiwa kuvipatia vijiji vyake vyote 60 nishati
ya umeme (ambayo ni sawa na asilimia 100) na hivyo kuongeza kasi ya wananchi
kujiendeleza kiuchumi katika sekta mbalimbali.
Hayo
yametolewa na ndg
Ismael Salum Meneja wa Shirika la Umeme Wilaya ya Siha tarehe 08/09/2018 katika kikao cha kamati ya
ushauri ya Wilaya ya Siha, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa
Halmashauri ya Siha.
Kikao
hicho chini ya Mwenyekiti Mhe. Onesmo Buswelu Mkuu wa Wilaya ya Siha walitoa
pongezi nyingi kwa uongozi wa shirika hilo Wilaya ya Siha kwa huduma bora
wanazoendelea kuzitoa kwa wananchi.
Meneja
wa shirika la umeme Wilaya ya Siha alieleza kuwa lengo la Serikali ni
kuhakikisha kuwa maeneo yote katika Wilaya ya Siha yanakuwa na huduma ya umeme ili
kuwezesha mpango wa Serikali ya Viwanda.
Wilaya
ya Siha imefanikiwa kusambaza umeme kwa vijiji 60 kati ya 60 vilivyopo na hadi
mwezi septemba, 2018 vitongoji 126 kati ya 169 vimepatiwa huduma ya umeme.
No comments:
Post a Comment